Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa akichangia na kufunga Semina maalum ya siku moja iliyoendeshwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuwaelimisha wadau wa vituo mbalimbali vya kutolea huduma za matibabu Mkoani Rukwa juu utaratibu wa Mfuko huo katika kutoa mikopo ya vifaa tiba, dawa na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za matibabu. Lengo kuu la utaratibu huo ulioanzishwa na Mfuko wa Bima ya Taifa ni kuboresha huduma za matibabu kwa wanachama wake na watanzania kwa ujumla. Semina hiyo imefanyika leo tarehe 02/03/2015 katika ukumbi wa RDC Mkoani Rukwa, Ndugu Pangisa amewaasa wadau hao kuchangamkia fursa hiyo kuimarisha huduma katika vituo vyao.
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Rukwa Ndugu Abdiel Mkaro akizungumza katika semina hiyo. Ndugu Mkaro alisema kuwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeanza utaratibu wa kuwakopesha wadau mbalimbali wanaotoa huduma za matibabu Mkoani Rukwa, lakini jambo la kushangaza wengi wao wamekuwa hawatumii fursa hiyo vizuri kwani baadhi yao wamediriki hata kutofuatilia maombi yao na kutelekeza barua zao ambazo wameshakubaliwa. Aliwaasa wadau hao kutumia fursa hiyo ili kuboresha huduma katika vituo vyao.
Mtoa mada mkuu katika Semina hiyo ndugu Yesaya Irira (Kulia) ambaye ni Afisa Mipango na Uwekezaji Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Makao Makuu akizungumza katika Semina hiyo ambapo amesema mikopo hiyo inatolewa kwa vituo vyote vya Serikali, vya Binafsi na vya Kidini kwa kigezo kikuu kuwa kituo hicho kiwe kimesajiliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kutoa huduma kwa wanachama wake. Aliongeza kuwa miongoni mwa taratibu za kupewa mkopo ni pamoja na Mkopaji kujaza fomu ya maombi ambapo kiwango cha Mkopo kitategemea wastani wa madai ya kituo kwa huduma zitolewazo kwa wanachama wa Bima ya Afya ambayo pia yatakuwa dhamana kuu ya Mkopo husika katika madai ya kila mwezi. Kwa Mkopo unaozidi Milioni tano Mkopaji atatakiwa kuweka dhamana yenye thamani ya mkopo na kwa upande wa mkopo wa kifaa tiba hufanyika kuwa dhamana ya mkopo mpaka marejesho ya Mkopo yatakapokamilika.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...