Na   Bashir  Yakub.

Upangaji  kama  upangaji  una  mambo  mengi.  Hii  ndio  sababu sheria  imegusa  eneo  hilo  pia.  Kila  mtu  anajua  kuwa upangaji  si  lazima  uwe  wa  nyumba  ya  kuishi tu bali  hata  ule  wa  maeneo  ya  biashara  pia.  Ipo  misuguano  mingi  ambayo  hutokea   katika  miamala  ya  upangaji  na upangishaji. Ipo  misuguano  inayotokana  na  ukorofi  tu  lakini  ipo  misuguano  inayotokana  na  kutojua  baadhi  ya  mambo  ya  msingi  na  ya  kisheria  kuhusu  dhana  nzima  ya  upangaji  na upangishaji . Leo  nitaeleza  mambo  mawili  tu   kuhusu  upangaji  na  upangishaji.

1.INARUHUSIWA  KUPANGA  NA  WEWE UKAMPANGISHA  MWINGINE.

Sheria  haimkatazi  mtu kupanga  sehemu  halafu   naye akaamua  kumpangisha  mwingine.  Hili  lipo  na  si  kinyume  cha  sheria  kufanya  hivi.  Na  zaidi  hata  huyu  aliyepangishwa  naye  anaweza  kumpangisha  mwingine  wa  tatu.  Yaani  ikawa  A  amempangisha  B  na  B  amempangisha  C   na  C  amempangisha  D  na  wote katika  eneo  hilohilo.  
Hii  yote  inaruhusiwa  na   upangaji  wa  kila  mmoja  unalindwa  na  sheria    na  kila mmoja  anapata  haki  zake kwa  nafasi  yake.  Kwa  mfano  kila mpangishaji  ataitwa  mwenye  nyumba  yaani  A  ataitwa  mwenye  nyumba  na  B  na  B  ataitwa  mwenye  nyumba  na  C  na  C  ataitwa  mwenye    nyumba  na  D.  Halikadhalika  kila  aliyepangishwa  ataitwa  mpangaji. 

Suala  la  msingi  sana  katika  upangaji  wa  namna  hii  ni  kuwa  ule  mkataba  wa  mwenye  nyumba  halisi  ambaye  ni mmiliki  kabisa  yule  A   uwe  unatoa  ruhusa  kwa    mpangaji aliyempangisha naye kuruhusiwa  kupangisha  mwingine   na  yule  mwingine  naye  mkataba  wake umruhusu  kumpangisha mwingine  na  mwingine  naye  mkataba  wake  umruhusu  kumpangisha  mwingine  iwe  hivyohivyo.   Ikiwa  mkataba  wa  mmoja haumruhusu  kupangisha zaidi  basi  huyo  asiyeruhusiwa   hawezi  kumpangisha  mwingine  na  akifanya  hivyo  itakuwa  kinyume    cha  sheria. Kisichowezekana  ni  kuwa huwezi kuwa  mpangaji  halafu  ukampangisha  mwingine  bila  kuwa  umeruhusiwa  kufanya  hivyo  na  mwenye  nyumba  katika  mkataba  wenu. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...