Kwa mwaliko wa Waziri wa Ardhi, Makaazi,Maji na Nishati wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Mheshimiwa Ramadhan Abdallah Shaaban, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi Maalum, Mark Mwandosya ametembeleaZanzibar kwa ziara ya kikazi. Pamoja na mambo mengine,Waziri Mwandosya amefungua rasmi Mradi wa maji wa Sebleni-Muungano-Sogea,SEMUSO.
Tanki la maji la Mradi wa Maji wa SEMUSO lililo Kibandamaiti,Zanzibai,Mradi uliozinduliwa na Waziri Mwandosya.
Waziri Mwandosya amepata nafasi ya kuhudhuria na kuhutubia mkutano wa wanachama wa CCM Wilaya ya Amani,mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini. Kulia kwa Waziri Mwandosya ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini, Ndugu Borafia Silima Juma.Kushoto kwa Waziri Mwandosya ni Ndugu Abdi Ali Mzee,Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani.
Waziri Mwandosya akifungua kisima cha maji cha Mradi wa SEMUSO.Nyuma yake mwenye mawani ni Mheshimiwa Mussa Mussa Mbunge wa Amani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...