Kwa mwaliko wa Waziri wa Ardhi, Makaazi,Maji na Nishati wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Mheshimiwa Ramadhan Abdallah Shaaban, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi Maalum, Mark Mwandosya ametembeleaZanzibar kwa ziara ya kikazi. Pamoja na mambo mengine,Waziri Mwandosya amefungua rasmi Mradi wa maji wa Sebleni-Muungano-Sogea,SEMUSO.
 Tanki la maji la Mradi wa Maji wa SEMUSO lililo Kibandamaiti,Zanzibai,Mradi uliozinduliwa na Waziri Mwandosya.
Waziri Mwandosya amepata nafasi ya kuhudhuria na kuhutubia mkutano wa wanachama wa CCM Wilaya ya Amani,mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa CCM Mkoa wa Mjini. Kulia kwa Waziri Mwandosya ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini, Ndugu Borafia Silima Juma.Kushoto kwa Waziri Mwandosya ni Ndugu Abdi Ali Mzee,Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani.
 Waziri Mwandosya akifungua kisima cha maji cha Mradi wa SEMUSO.Nyuma yake mwenye mawani ni Mheshimiwa Mussa Mussa Mbunge wa Amani.
Baada ya kufungulia bomba(mfereji) la maji ya Mradi wa SEMUSO,Kibandamaiti,Zanzibar,Waziri Mwandosya amtwisha ndoo ya maji Ndugu Ali Magoha, Mjumbe wa Kamati ya Mradi wa SEMUSO, kuashiria kuyafikisha maji kwa watumiaji.Nyuma ya Waziri Mwandosya kutoka kushoto ni ;Mheshimiwa Muhammad Seif Khatib,Mbunge wa Uzini;Mheshimiwa Ramadhan Abdallah Shaaban,Waziri wa Ardhi,Makaazi,Maji na Nishsti wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar;na Mheshimiwa Mussa Hassan Mussa,Mbunge wa Amani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...