MAULID BARAKA KITENGE WITH CO HOST  IBRAHIM MASOUD “MAESTRO” NA OMAR KATANGA.
WACHAMBUZI  OSCAR OSCAR,  MUSSA KAWAMBWA  NA SUDI  MKUMBA
WATAYARISHAJI : YUSUPH MKULE, FRANCIS MHANDO, DR PANJUAN NA  WENGINEO....

1.    MAULID KITENGE NI NANI?,
Huyu ni mtangazaji nguli wa Sports Tanzania, aliyetumia kipindi cha miaka kumi na nne(14) kwenye moja kati ya vituo maarufu nchini Tanzania, na mwanzilishi wa Sports E FM Radio, ambae anafahamika sana kwa utangazaji wake maridhawa, na maswali yenye kutia kashkashi ambayo huleta mvuto mkubwa kwa wasikilizaji..na ambae anaamini kile anachokiamini yeye, na akiwa ni mwenye kujiamini kwa mapana na marefu kitu kikubwa alichonacho Kitenge ni hupenda kushauriwa na kumsikiliza kila mwenye kuhitaji kujifunza kutoka kwake.
2.    IBRAHIM “MAESTRO” MASOUD ..
Mtangazaji mwingine Nguli wa sports Tanzania, akiwa muongozaji na mchambuzi mahiri wa sports kwenye Radio na Television, uzuri wa huyu bwana aliwahi kuwa mchezaji wa klabu kadhaa za ligi mbalimbali Tanzania bara na Visiwani, na ambae pia ni mwalimu wa soka wa Ngazi ya kati, na mwenye taaluma ya soka la vijana aliyebobea, akiwa nauzoefu wa miaka isiyopungua kumi na minne (14) kwenye kiwanda cha habari za michezo Tanzania... 
3.    OMARY KATANGA…
Mtayarishaji na muongozaji pia muanzilishi wa E-Sports ya E-fm mbali na umahili wake katika sports, lakini pia ni msomaji mzuri wa Taarifa za habari, anatumia  style ya kipekee inayopendwa na wasikilizaji  ya kwenda speed wakati wa kutangaza  michezo, ana maswali ya mtego yenye kuleta burudani masikioni mwa wasikilizaji wakati akifanya mahojiano na watu waliomo kwenye familia ya michezo, ni mtangazaji makini sana kwa kila akipelekacho hewani.
4.    OSCAR OSCAR..
Kitaaluma ni mwalimu, na ambae ameibuka kuwa mmoja kati ya wachambuzi wanaokuja juu sana kwenye michezo Tanzania kutokana na kuwa mfuatiliaji sana wa masuala ya soka,  na mara nyingine hufanya  uchambuzi kwenye vipindi vya TV kama Kabumbu show, na uchambuzi wa mechi za Premier ya England, kwenye kituo cha Utangazaji  cha Kimataifa-BBC.
5.    MUSSA KAWAMBWA..
Ni mchambuzi na muaandaji wa kipindi cha michezo hapa 93.7 EFM mwenye uzoefu wa hali ya juu katika tasnia hii akiwa amepita katika vituo mbalimbali vikubwa hapa nchini, pia ni muandaaji wa kipengele cha HISABATI ndani ya Sports Headquarters na Chakuchabo. Sauti yake ya kuvutia pamoja na historia kubwa aliyonayo hasa katika soka la barani Ulaya ni moja kati ya vitu vinavyomfanya awe wa kipekee. Mwisho kabisa ni uelewa wake juu ya michezo kama Tennis, Cricket, Rugby, Masumbwi na Langalanga. 
1.    FRANCIS MUHANDO.
Ni mtayarishaji na reporter  wa vipindi vya michezo hapa 93.7 EFM, unayeweza kumsikia katika kipengele cha Robo saa ya nguvu akifanya mahojiano na wanamichezo mbalimbali. 
2.    YUSUPH MKULE.
Mtayarishaji na muongozaji wa vipindi vya michezo hapa Efm, E.Sports & Sports HQ na amekuwa mtangazaji wa michezo tangu mwaka 2009 kwakufanya kazi katika redio mbalimbali  hapa nchini Tanzania. Pia amewahi kuwa msimamizi wa vipindi katika mmoja ya redio aliyowahi kufanya kazi katika mikoa ya nyanda za juu kusini mwa Tanzania.  
Kwaujumla ni kati ya watangazaji na waongozaji wa vipindi vya michezo  ambaye  kwasiku za usoni atakuwa moto wa kuotea mbali na hilo analithibitisha katika kipinchi cha E.Sports na Sports HQ hapa E.FM.
3.    SUDI MKUMBA.
Mtayaarishaji na mchambuzi wa vipindi vya  E Sports na Sports HQ ni ni miongoni mwa walioanzisha vipindi hivi  vya michezo hapa 93.7 EFM pia ndiye mchambuzi wa kipengele cha michezo katika kipindi cha UBAONI kinachoongozwa na mtangazaji Gadner G Habash.
Ni mchambuzi anaechipukia na anaekuja kwa kasi kubwa katika tasnia hii ya uchambuzi na uandaaji wa vipindi vya michezo radioni.
SPORTS HEADQUATERS..
Ni show ambayo imekusanya michezo yote duniani, ambayo Platfom yake ni E Sports, ikiwa na Vipengele mbalimbali kama vile habari za nyumbani na uchambuzi yakinifu, Robo saa ya nguvu ya kwanza ambayo inahusisha mahojiano ya wanamichezo mbalimbali, Hisabati, Maswali ya Dr Panjuani, Robo saa ya pili ya nguvu kwa habari za kimataifa, ikiwemo Soka, Basketball, Boxing,Tennis, Rugby,Formula 1,Golf, Cricket, Netball na kadhalika, na mwisho kuna kitu kinaitwa, Cha kuchabo,,ambacho kinapekua habari zilizojificha.
Pamoja na yote hayo, bado pia kuna burudani ya kutosha ua muziki uliopangika vizuri toka kwa ma Dj waliobobea kwenye Burudani, RDJ’S.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 15, 2015

    MKUU HII IMETULIA SANA!! UNAWEZA KUWEKA PICHA ZAO/PICHA ZA MUHUSIKA JUU YA KILA MAELEZO YAKE CHINI YA JINA LAKE ...Tupate kuwajua watu hawa Mahiri!!! Asanteni sana efm kwa mapinduzi makubwa mliyoleta

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 15, 2015

    That what you call all stars AKA dream team,what a combination?kudos to efm management keep good work.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...