DENNIS SSEBO NA  ADELLA TILLYA.
 1.     12:00 HADI SAA 3:00 KAMILI ASUBUHI UNAPATA
" JOTO LA ASUBUHI" ILI KUKUANZISHIA SIKU

DENNIS SSEBO  NI NANI?
Ssebo  ni moto ama baruti ya kipekee katika masuala ya Radio, akiwa ni muhitimu wa mambo ya sheria na ana  shahada ya udhamiri katika mambo ya mawasiliano ya Umma lakini akiwa na ufahamu  na mapenzi zaidi  upande wa Radio na TV.
Ssebo amekuwa kwenye Tasnia hii kwa muda mrefu akiwa na uzoefu wa kufanya kazi Zaidi  Radio na Tv kwa muda wa miaka 15, lakini pia amekuwa akisaidia kwakiwango kikubwa sana katika  kuboreha vipindi vya Radio na Tv nchini Tanzania.
Wapo watu wachache ambao wanatambua uwezo wake wakuburudisha na kufundisha,  Zaidi amejulikana kuwa ni mtu wa masihala au utani lakini Dennis Ssebo ni mtu makini anayejitambua na muda wake mwingi ameutolea kwenye kusoma na kufanya tafiti mbalimbali.
Ssebo anasema “ Ninasema kile ambacho ninakiona, lakini kama hukubaliani nacho ni uamzi wako”  Mpende au umchukie lakini kwa hakika utacheka, utashangaa na utajifunza kitu  unapomsikiliza radioni.
Ssebo ni mtangazaji ambaye EFM Radio imempa nafasi ya kukuamsha na kuwa nawe kila siku asubuhi  kuanzia saa kumi na mbili hadi saa tatu kamili asubuhi , Jumatatu hadi ijumaa. 

MJUE ADELLA TILLYA 
Na hiyo sauti ya kike unayoisikia kila siku pamoja naye asubuhi, si ya mwingine bali ni mwanadada  shupavu ( Iron Lady) ambaye huwezi kumpata sehemu yoyote Zaidi ya Efm Radio.
Hapa namzungumzia Adella Tillya, ambaye  ni mtayarishaji wa Kipindi cha Joto la Asubuhi na juhudi zake mara nyingi zinatambuliwa sana na Ssebo ambaye amekuwa akimwambia  “ katika wewe ninaona taarifa”
Adella amekuwa na uzoefu wa kuandaa na kutangaza  na ni miongoni mwa watangazaji wa chache ambao mpaka sasa wameweza kumshika Ssebo.
Ni ajabu hata katika ofisi za Efm amekuwa akiitwa mwanamke shupavu na hata akisikika hewani  akicheka lakini haimanishi kuwa ni mwanamke wa kawaida.
Ni watu hawa wawili,  watundu,  lakini wakiwa na taarifa za kutosha za mambo mbalimbali ambao kwa pamoja wanakupa Joto la Asubuhi.
Katika kipindi cha Joto la Asubuhi, utapata  habari za ndani na Nje ya nchi, uchambuzi wa magazeti ya ndani na nje, mada mbalimbalimba kuhusiana na mambo yanayoendelea ulimwenguni bila kusahau zawadi zitolewazo kwa wasikilizaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...