Bondia wa Kimarekani,Floyd Mayweather Jr akimrushia konde kali mpinzani wake, Manny Pacquiao wa Philipines wakati wa mpambano wao wa kihistoria na uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu na watu wengi Duniani kote, uliopigwa mapema leo kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa MGM Grand Garden Arena, jijini Las Vegas, Marekani. Bondio Floyd Mayweather ameshinda mchezo huo kwa point 118-110, 116-112, 116-112 kutoka kwa waamuzi wa mchezo huo na kunyakuwa mkanda wa WBO huku akiifanya rekodi yake ya kutopigwa kufikia michezo 48.
Mchezo ulikuwa ni mkali sana na Mabondia wote walikuwa wakirushiana makonde kwa zamu.
haya angalieni wenyewe hasa wale wanaosema jamaa kabebwa.
Mabondia Floyd Mayweather na Manny Pacquiao wakifurahi pamoja mara baada ya mpambano wao wa kihistoria uliopigwa mapema leo kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa MGM Grand Garden Arena, jijini Las Vegas, Marekani.

Bondia Floyd Mayweather Jr akiwa na mikanda yake na tuzo aliyoshinda katika michezo mbali mbali 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...