Kama
utakuwa na kumbukubu nzuri kipindi cha nyuma kidogo ulikuwa ukiingia kwenye
mtandao utakuta domain nyingi ziko kwa namna ya jinafulani.com alafu baada ya
muda tukaanza kuona jinafulani.co.uk ila hapakuwa na jinafulani.co.tz. Hilo
lime badilika na kwa takwimu
za sasa kuna takribani domain 10,000 zinazoishia na .tz
ambazo zimesajiliwa na tzNIC moja kwa moja au kupitia wakala wao.
Tanzania
Network Information Centre (tzNIC) ni msajili wa domain zinazo ishia na .tz.
Hivyo pale unapo taka kusajili domain ambayo inaishia na .tz hawa ndio wahusika
wakuu. tzNIC wanasimamia mfumo ambao una onyesha barua pepe yani email na
servers zote zinazo ishia na .tz na zilipo. Tanzania Network Information Centre
nishirika lisilo la kutafuta faida (nonprofit) ambalo lilianzishwa na kusajiliwa
mwaka 2006 kwaajili ya kusimamia na kutekeleza shuguli zote zinazo husiana na
Tanzania country code Top Level Domain (.tz ccTLD).
tzNIC ni limited company
(kwa dhamana) ambayo ina waanzilishi wawili ambao ni TCRA ambae ni mdhibiti
mkuu wa maswala ya mitandao Tanzania na TISPA (Tanzania Internet Service
Provider Association) ambae ni sehemu ya chama cha ISP (Internet Service
Provers Association).
Lengo la tzNIC
Lengo
kuu la tzNIC ni kukuza matumizi ya majina ya domain yanayo ishia na .tz pamoja
na kulinda maslahi ya walio sajiliwa kwa kuwapa database ambayo ina ulinzi wa
kutosha na unafuu. Kwa kufanya hivyo huwapa watumiaji fursa ya kuonekana dunia
nzima, wana brand huduma yako na muonekano wa kitanzania, kuongeza ushindani wa
biashara yako ndani na nje ya Tanzania, kuwezesha domain yako ulio sajili
kupata watembeleaji wengi wa ndani ya nchi ya Tanzania, na kukuza utumiaji wa
mtandao katika biashara.
Wako
wapi
Head office za tzNIC (Tanzania Network Information
Cetre) ziko Suite #4 Ground Floor, of LAPF
Millenium Towers, at the New Bagamoyo Road, Dar es Salaam na namba zao za simu
ni +255 22 2772659 fax: +255 22 2772660 na email address ni: info@tznic.or.tz
hivyo pale unapo taka ku register domain yako au una tatizo linalo husiana na
usajili wa domain usisite kuwasiliana nao au
kuwatembelea.
Website;
http://www.tznic.or.tz/
Facebook; https://www.facebook.com/tznic
Twitter;
https://twitter.com/tznic
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...