Na Niccomeditz
KUTOKANA
na mvua kubwa zilizonyesha karibu maeneo yote ya nchi na kuleta maafa
hususan katika jijin la Dar es Salaam Kampuni ya Aqua Cool Ltd
Watengenezaji wa maji safi ya Kisima Pure Drinking Water imetoa msaada
wa mavazi ya kujikinga na mvua ya mpira (ponchos) kwa wakazi wa wilaya
ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Msaada huo ulitolewa na uongozi na wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa
makundi mbalimbali kama watembea kwa miguu, mama lishe , waendesha
bodaboda na wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini wakati wa kutoa msaada huo
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Ali Dhanji alisema kampuni
imefanya hivyo kama sehemu ya shukrani kwa jamii, kuwajali wateja wao
pia kwa wananchi wa kawaida walioathirika na kutatizwa na kadhia
ya mvua inayoendelea kunyesha .
Aliongeza kusema wamefanya hivyo ili kuwarejeshea urahisi wa kufanya
shughuli zao ambazo kutokana na maafa yaliyosababishwa na mvua na
kuwakwamisha kuendelea na shughuli za kujipatia kipato kwa muda hivyo
kuyumba kiuchumi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...