Na Niccomeditz

KUTOKANA na mvua kubwa zilizonyesha karibu maeneo yote ya nchi na kuleta maafa hususan katika jijin la Dar es Salaam Kampuni ya Aqua Cool Ltd Watengenezaji wa maji safi ya Kisima Pure Drinking Water imetoa msaada wa mavazi ya kujikinga na mvua ya mpira (ponchos) kwa wakazi wa wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Msaada huo ulitolewa na uongozi na wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa makundi mbalimbali kama watembea kwa miguu, mama lishe , waendesha bodaboda na wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama machinga.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini wakati wa kutoa msaada huo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Ali Dhanji alisema kampuni imefanya hivyo kama sehemu ya shukrani kwa jamii, kuwajali wateja wao pia kwa wananchi wa kawaida walioathirika na kutatizwa na kadhia ya mvua inayoendelea kunyesha .

Wafanyakazi wa kampuni ya maji ya Kisima AQUA COOL LTD wakitembea wakiwa wamevaa mavazi ya kujikinga na mvua ya mpira (ponchos) Kushoto ni Meneja Masoko Bw. Sachin Smart , katikati ni Mkurugenzi Mkuu Bw.Ali Dhanji na kulia ni Meneja wa uzalishaji Bw. Mohamed Saleh .
Aliongeza kusema wamefanya hivyo ili kuwarejeshea urahisi wa kufanya shughuli zao ambazo kutokana na maafa yaliyosababishwa na mvua na kuwakwamisha kuendelea na shughuli za kujipatia kipato kwa muda hivyo kuyumba kiuchumi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...