Na  Bashir  Yakub.
Kutokana  na  maendeleo  ya  biashara  duniani  kote  imekuwa  ni vigumu  sasa  kufanya  biashara  nje  ya kampuni.  Hii  ni  kwasababu  kila  kampuni  au  taasisi  utakayotaka  kufanya  nayo  biashara   iwe  kununua  kwao  au  kuuza  kwao  basi  kitu  cha  kwanza  watakachokwambia  ni  kuwa  hatufanyi  biashara  na watu  binafsi.  

Zipo  biashara  ambazo    watu  wengi  bado  wanazifanya  nje  ya  kampuni   lakini  ukweli  ni  kuwa  biashara  hizo  kwa ulimwengu  wa  biashara  wa  sasa   ni  za kienyeji   na  tija  yake  bila  shaka  ni  ya kusuasua.  

Kwa hali  ilivyo sasa hadi   migahawani   unaposupply  mayai  au  kuku  wa  nyama n.k  sio muda mrefu   watakwambia  sasa tunahitaji  kampuni  ndio isupply na  sio mtu  binafsi .  Kama  hali  ni hiyo   nini  basi   mjasiriamali  wa  leo  afanye.

1.NINI  MJASIRIAMALI  AFANYE   KWA SASA.

Kilio  cha  mjasiriamali  makini   siku  zote  huwa   hali  na  wala  halali  isipokuwa  anawaza  nini  kesho  afanye  ili  biashara  zake  zitoke  hapo zilipo    na  kwenda  hatua   nyingine  mbele.  Mjasiriamali  mwenye  mawazo  hayo   ndiye  huanza  na  mtaji  wa  elfu  kumi  baada  ya  mwaka  zikazaa  milioni  tano na  baada  ya  miaka  akamiliki  milioni  mia. Huyu  huitwa   mjasiriamali  mwenye  fikra  chanya( positive thinking enterprenuer) . Nimesema  hapo  juu  kuwa   hali  ya  biashara  imebadilika   kwa  namna  ambayo  wadau  wa  biashara   wamejielekeza  katika  kufanya  kazi  na  makampuni  badala  ya  watu  binafsi  kama  tulivyozoea.

  Swali  la  nini  mjasiriamali  afanye  katika  hali  hiyo   jibu  lake  ni  kuwa  mjasiriamali  naye  abadilike. Kama  mwaka  jana  ulifuga  kuku  wewe  kama  wewe binafsi  basi  leo  fuga  kuku chini  ya  kampuni,  kama  mwaka  jana   ulilima  mihogo  Chanika  na kuuza  sokoni  wewe  kama wewe  basi  leo  lima  mihogo  na  uza  lakini  si kama wewe  binafsi  isipokuwa  chini  ya  kampuni.   Una  tigo pesa  yako,  duka, liwe  la  mavazi  au  bidhaa  nyingine, fundi  fenicha, unamiliki  taxi, fundi  cherehani,   na  kila  kitu  unachofanya   kwa  ajili  ya kipato   basi  sasa  ni  wakati   kumiliki  kitu hicho  kupitia  kampuni. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...