Huwezi  kufikiria  umiliki  wa kampuni  kabla  ya kufikiria  kuhusu  mtaji  wa  kampuni. Mtaji  wa kampuni ni  suala  nyeti  kwa  wenye  wazo  la  kumiliki  kampuni  au  wanaomiliki  kampuni  tayari.  Mtaji  ndio  kila  kitu  katika  kampuni. Tangu  unapokuwa  katika  harakati  za  kusajili kampuni  utalisikia  neno  hili  mtaji  karibia katika  kila  hatua  unayopita. Niseme  mapema  kuwa  mtaji  mdogo  ndio  kampuni ndogo  na  mtaji  mkubwa  ndio  kampuni  kubwa.  Kwa  hili  mitaji  imegawanyika  mara  mbili upo  mtaji  wa  maandishi unaokuwa  kwenye   katiba  na  waraka  wa  kampuni( MEMAT)   na  upo  mtaji  wa  mali  halisi ( physical assets).
Mtaji  wa   unaokuwa  kwenye  nyaraka nilizotaja  mara  nyingi  hautambulishi  ukubwa  au udogo  wa  kampuni. Hii  ni  kwasababu  mtaji  huu  huwa  ni  maandishi  tu na  yawezekana  kiwango  cha fedha  kilichoandikwa   humo  kama mtaji   hakipo  kabisa  katika  kampuni.  Hivyo  mtaji  wa  aina  hii  hauna  uhusiano wowote   na  ukubwa  au  udogo  wa  kampuni.  Kwa  upande  wa  mtaji  wa  mali   halisi   huu  ndio  mtaji  ambao  huweza  kutambulisha  ukubwa  au  udogo  wa  kampuni.  Hii  ni  kwasababu mtaji  huu  huwa   sio  maneno  tu  au maandishi  bali  mali kwa  maana  ya  mali . Na  kisheria  mali  kama  mali  za  kampuni  ndio  mtaji  wa  kampuni  na  ndio  nitakaozungumzia  hapa.  Nitazungumzia  mtaji  lakini  zaidi   ni  kujua  mtaji  hujumuisha  nini. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...