Na  Bashir  Yakub.
Mara  nyingi  nimeandika  kuhusu  ardhi  hususan   viwanja  na  nyumba.  Katika  kufanya  hivyo  mara  kadhaa  nimejaribu  kuwatahadharisha  watu namna  mbalimbali  ya  kisheria ya kuepuka   kuingia  katika  migogoro  ya  viwanja  na  nyumba  hasa  wakati  wa  kununua( wanunuzi). 

 Nimewahi  kueleza  namna  au  vitu  vya  msingi ambavyo  hutakiwa  kuwa  katika  mkataba  wa   ununuzi  wa  nyumba  au  kiwanja. Nikaeleza  umuhimu  wa  kila  kimoja   na nikasisitiza  kuwa  atayekuwa  amenunua  ardhi na  mkataba  wake  ukajaaliwa   kuwa  na  vitu  hivyo  basi  si  tu  atakuwa  amefanya  manunuzi  bora  lakini  pia  atakuwa  amefanya manunuzi  yanayokubalika  kisheria. 

Ifike  hatua  watu waelewe kuwa  migogoro  mingi  ya  ardhi  huanzia  na  kutokuwa makini kwenye  manunuzi. Kutokupata  ushauri  wa  kisheria   ikiwa  ni  pamoja  na  kutopitia  hatua   za  msingi za kisheria  kabla  ya  manunuzi,  kuandikiwa  mikataba ya  manunuzi  isiyokidhi  vigezo  vya  kisheria  ikiwemo  ile  ya  serikali  za  mitaa  ambayo  hairuhusiwi  kabisa kisheria  ni  kati  ya sababu chache  kati  ya  nyingi  zitakazokupelekea  uingie  katika  mgogoro.  Leo  nitaeleza  hatua  moja   ya  msingi  sana  ambayo  hutakiwi ufanye  manunuzi  ya  ardhi  bila  kuipitia.

 1.HATUA  TANO  ZA  KUFUATA   UNUNUAPO   NYUMBA/KIWANJA.  

Ziko  hatua  tano  muhimu  za  kupitia  pale  unapo kuwa  katika  mchakato  wa    kununua  ardhi. Umuhimu  wa  hatua  hizi  ni  kuwa  kwanza  kabisa  si  rahisi  kujikuta  katika  mgogoro  unapokuwa    umezipitia.  Lakini  pili  hata  bahati  mbaya   utokee  mgogoro   basi  wewe  uliyepitia  hatua  hizo  utakuwa  salama  na  kama  ni  kesi  basi  wewe  upo  katika  mazingira  mazuri  ya  kushinda.  Hatua  ya  kwanza  huitwa  hatua  kabla  ya  mkataba( pre contractual  stage).  

Hatua  hii inayo  mambo  yake  ya  msingi  na  ya  kisheria     ambayo  kuyafuata  kwako  kwaweza  kukuweka  mbali  na hatari  ya  kununua  ardhi  yenye  mgogoro  au  itayokuingiza  katika  mgogoro  . Hatua  hii  ndiyo  nitakayoeleza   kama  msingi  wa  makala  ya  leo  kama  tutakavyoona.  Kabla  ya  kueleza  hatua  hiyo  ni  vema  pia  nikazitaja  hatua  nyingine   japo  kwa  ufupi. Hatua  ya pili  huitwa  hatua  ya  mkataba( contractual  stage). Hii  ni  hatua  ya  kupitia  na  kujiridhisha  na  mkataba    wa  manunuzi  ikiwa  ni  pamoja  na  kuusaini. Hatua  ya  tatu  huitwa  “pre completion  stage”,  hatua  ya nne  huitwa  hatua  ya  kumalizia ( completion stage)  na  hatua  ya  tano  na  ya  mwisho  huitwa  hatua  baada  ya  kumalizia ( post  completion  stage). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...