Na   Bashir    Yakub.

Mara  nyingi  unapounda  kampuni   huwa  ni  lazima  kueleza  katika  zile  Memorandum  kuhusu  ukurugenzi  na  wakurugenzi.  Huwezi kusajili   kampuni  ikiwa  memorandum  zako  hazioneshi  lolote  kuhusu    hilo. 

Kimsingi  nitaeleza  machache  japo  yapo   mengi kuhusu  ukurugenzi  na wakurugenzi  katika  kampuni.  Kwa  kampuni  zetu  ndogo ndogo  za  kijasiriamali  mara  zote  wakurugenzi  ndio  hao hao  wamiliki  na  ndio hao  hao  wana  hisa.  Niseme  mapema  tu kuwa si kosa  kuwa  hivyo  isipokuwa  yatupasa  kufahamu   kuwa  kuna  tofauti  kati  ya  wakurugenzi, wanahisa,  na  wamiliki.  

Wakurugenzi  wanaweza  kuwa  watu  wa  kuajiriwa    na  wasiwe na  uhusiano  wowote  katika  umiliki.  Unakuta mtu ameajiriwa   tu  kama  mkurugenzi  kwa  ajili ya  kuendesha  kampuni  pengine  kutokana  na  elimu  yake,  uwezo  wake,  uzoefu  n.k.  Mwanahisa  naye anaweza  kuwa  mwanahisa  tu   na asiwe mkurugenzi  na  mmiliki  anaweza  kuwa   mmiliki tu  na asiwe  mkurugenzi.   Isipokuwa  tu mmiliki  lazima  awe  mwanahisa  kwasababu  hakuna  namna  ya  kufikia  kuwa  mmiliki  wa kampuni  bila  kuwa  mwanahisa. 

Hivi  ni  vitu ambavyo  huwezi  kuvitenganisha. Mara  nyingi wanaotenganisha umiliki, ukurugenzi  na  uanahisa  ni  wenye  makampuni  makubwa.  Makampuni  yetu    madogo  ya  kufuga  kuku   mkurugenzi  ndiye  mmiliki  na  ndiye  mwanahisa.  Tutaona  baadhi  ya mambo   hapa   chini  kuhusu   ukurugenzi  wa  kampuni.

1.NINI  MAANA  YA   MKURUGENZI.

Sheria  ya  Makampuni  tunayotumia  hapa  nchini  imetoa  tafsiri  nyepesi  ya  maana ya  mkurugenzi  kwa  kusema kuwa mkurugenzi    ni  mtu  yeyote  ambaye   amepewa  nafasi  ya  ukurugenzi.  Sheria  hiyo  inasema  hivyo  kwa  kumaanisha kuwa  ili  umwite   mtu  mkurugenzi  au  hapana  itategemea  na    na  majukumu  anayotekeleza  katika  kampuni.  Ni  majukumu  tu  ndio  yatamtambulisha  mtu  kama  mkurugenzi.  

Hii  ina  maana  yawezekana  mtu   akawa  anaitwa  mkurugenzi  lakini  hana  majukumu  ya  kiukurugenzi.  Kwa  tafsiri  hii  huyu   kisheria  sio  mkurugenzi.  Mwingine  yaweza   kuwa  anaitwa  mwenyekiti  lakini  akitekeleza  majukumu  ya  kiukurugenzi.  Huyu  kisheria  atatambulika  kama  mkurugenzi. Kwa  hiyo  kwa  kujibu  wa  tafsiri  hii  kumbe tunaona  kuwa   ukurugenzi  ni  majukumu  wala  sio  jina. 

Pamoja  na hayo baadhi  ya  Mahakama   huko Wingereza  zimekuwa  zikitoa  tafsiri  mbalimbali  kuhusu  maana ya  ukurugenzi  ambapo  tafsiri  iliyokubalika  sana  ni ile  inayosema kuwa mkurugenzi  ni mtu  ambaye  ana  mamlaka  ya  kimwongozo,  kimaadili  na  kiutawala  katika  shughuli  zote  na  za  kila  siku  za  kampuni. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...