Mwandishi mkongwe wa habari, Kyaloeichi Oko Kessy (62) amefariki dunia usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake Pugu jijini Dar es Salaam.

Mpwa wa marehemu Tumaini Msengi amesema hayo leo kuwa marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu kwa muda mrefu na amekuwa akitibiwa katika hospitali mbalimbali za jijini Dar es Salaam hadi jana ambapo mauti yalimkuta.

Kabla hajaanza kuugua Kessy alikuwa mwandishi wa kujitegemea akiandika zaidi uchambuzi na makala katika vyombo mbalimbali vya habari nchini yakiwemo magazeti ya Motomoto,Shaba,Rai, na mengineyo mengi pia alikuwa ni mtunzi wa vitabu vya aina mbalimbali.

Msengi ameeleza kuwa marehemu ameacha watoto wawili na mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa mdogo wake Chanika nje kidogo ya jiji na mazishi yanatarajiwa kufanyika wiki ijayo.

Marehemu ni mzaliwa wa kijiji cha Rosho Kilema mkoani Kilimanjaro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...