Mgombea
anayetajwa kuwania kiti cha ubunge katika jimbo la Arusha mjini kupitia
Chama Cha Mapinduzi(CCM),Thomas Munisi amewataka wagombea wa chama
hicho kutochafuana kwenye majukwaa na vijiwe bali wafanye kampeni za
kistaarabu.
Munisi,ambaye pia ni mkurugenzi wa kampuni ya
Kilimanjaro Millenium Printers(KPML) yenye makao makuu yake jijini
Arusha alitoa kauli hiyo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari
jijini hapa kuhusu uamuzi wake wa kugombea ama la.
Hadi sasa jijini
Arusha jumla ya wagombea saba wamejitokeza kutia nia ya kugombea jimbo
la Arusha mjini kupitia CCM ambao ni Kim Fute,Mustapha
Panju”Bushbuck”,Phillemon Mollel”Monaban”,Victor Njau,Edmund
Mgemela,David Rwenyagira pamoja na mbunge wa zamani wa jimbo hilo Felix
Mrema.
Akiongea katika hoteli ya Palace iliyopo jijini Arusha
alisema kuwa si vyema wagombea wa CCM kuanza kampeni za kuchafuana
kupitia kwenye vijiwe na majukwaa kwa kuwa haileti picha nzuri ndani ya
chama.
“Mimi nashangaa wagombea wanapita huko vijiweni na
kuanza kuchafua wenzao wakati sote tunajenga nyumba moja”alisema Munisi
ambaye pia ni mmiliki wa kamuni ya madini ya Tom Gems
Hatahivyo,alisema
kuwa ndani ya CCM watajitokeza wagombea mbalimbali lakini mwisho wa
siku ni mgombea mmoja tu atakayepitishwa na chama kwa lengo la
kupeperusha bendera ya CCM.
Akizungumzia uamuzi wake wa
kugombea jimbo hilo au la alisema kuwa kwa kuwa taratibu ndani ya chama
zimeshatangazwa na muda ukiwadi atafanya maamuzi sahihi kwa maslahi ya
wakazi wa jimbo la Arusha mjini.
Mgombea anayetajwa kuwania kiti cha ubunge katika jimbo la Arusha mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM),Thomas Munisi (Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...