Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
TUME ya Taifa ya Uchaguzi Nchini(NEC),inatarajia kuchunguza mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi na kuyagawa kwa ajili ya uchaguzi wa Wabunge unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.

Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa NEC,Jaji Mstaafu Damian Lubuva wakati alipokutana na viongozi wa Vyama vya Siasa kujadili masuala mbalimbali ya Tume katika kuelekea uchaguzi Mkuu.

Amesema  ugawaji wa Majimbo,Tume imezingatia vigezo mbalimbali ikiwemo idadi ya watu,upatikanaji wa mawasiliano hali ya kijiografia na vigezo vingine kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Rais na Wabunge ya mwaka 2010.

Jaji Lubuva amesema ugawaji wa majimbo hufanyika kila baada ya miaka 10 na ugawaji huo utafanywa kabla ya Oktoba na hii inatokana na kuongezeka kwa idadi ya watu katika majimbo na kuona kuna umuhimu wa kugawa majimbo kwa mujibu wa sheria.

Aidha amesema ugawaji wa majimbo sio kwa kuangalia idadi ya watu,bali upatikanaji wa mawasiliano inayojumuisha miundombinu,simu na vyombo vya habari kwa ajili ya kupata mwakilishi atakayeharakisha maendeleo katika eneo husika.

Lubuva amesema kuwa uchaguzi mkuu utafanyika kama ulivyokuwa umepangwa kutokana na zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linaendelea katika mikoa iliyoainishwa.
  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC),Jaji Mstaafu,Damian Lubuva akizungumza katika Mkutano wa Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini kujadili masuala mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka  huu uliofanyika leo katika Hoteli ya New Afrika Jijini Dar es Salaam,Kushoto ni Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar Hamid Mahmoud Hamid.
  Kamishina wa Tume ya uchaguzi,Profesa Amon Chaligha akizungumza katika mkutano wa viongozi vyama vya Siasa katika ukumbi wa Hoteli ya New Africa leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Julius Malaba.
 Mwenyekiti wa Taifa Chama cha Wananchi (CUF), profesa Ibrahim Lipumba akichangia maada katika Mkutano wa Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini kujadili masuala mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka  huu uliofanyika leo katika Hoteli ya New Afrika Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Chama cha Tanzania Labour Part (TLP),Nancy Mrikaria akitoa ufafanuzi juu ya viti maalumu Bungeni katika Mkutano wa Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini kujadili masuala mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka  huu uliofanyika leo katika Hoteli ya New Afrika Jijini Dar es Salaam.(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...