Mtayarishaji wa filamu na mwimbaji wa siku nyingi Jennifer Mgendi anakusudia kuachia filamu yake ya “Nipo Studio” mapema wiki hii. Akiongea na blogu hii Jennifer amesema filamu hiyo imekamilika kwa kila kitu na itaingia sokoni wiki hii ikiwa imewashirikisha wasanii mbalimbali akiwamo shosti wake wa siku nyingi Bahati Bukuku, Bibi Esta, Hassan Mbangwa, Gwamaka Kametta na wengine wengi.
Jennifer amesema filamu hii inazungumzia changamoto mbalimbali anazokutana nazo Bibi Esta pale anapokuwa na ndoto ya kuwa mwimbaji huku umri na kipato vikiwa kikwazo kwake.
Wakati huo huo Jennifer amesema maandalizi ya tamasha lake la uzinduzi wa video ya Wema ni akiba yanaendelea vizuri na tamasha hilo litafanyika kama ilivyopangwa tarehe 28 Juni katika kanisa la DCT Tabata Shule huku Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Assemblies of God , Dr. Barnabas Mtokambali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...