MFUKO wa Pensheni wa PPF, umepewa cheti cha ubora wa utoaji huduma kimataifa kwa wananchi (ISO) baada ya kukidhi mashariti na vigezo.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio alitoa taarifa hiyo leo Ijumaa  na kusema kuwa walipewa tangu Machi 28, mwaka huu.


Alisema wamepewa cheti chenye namba 9001:2008 na kuanzia mwezi Mei, mwaka huu huduma za PPF zinaza kutambulika kimataifa.

“ISO walikuja nchini wakatukagua wakalidhika na viwango vya huduma zetu tunazotoa na wakatupatia cheti cha ubora,” alisema Erio.


Alisema kwa sasa wanachma wa PPF wategemee kupata huduma bora pamoja na uwajibikaji ulio bora.

Alisema kila baada ya miezi sita ISO watakuwa wanatembelea PPF na kukagua kama huduma bora bado zinatolewa, na kila baada ya miaka mitatu PPF watatakiwa ku-renew maombi ya ISO.


Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (katikati) akizungumza wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya cheti cha ubora wa utoaji huduma kimataifa kwa wananchi (ISO) walichokipata baada ya kukidhi mashariti na vigezo

Mameneja wa PPF, na waandishi wa habari wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio juu ya tuzo hiyo
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (katikati), Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Julius Mganga (kushoto) na Mkurugenzi wa Udhibiti Majanga (risk management), Ufoo Swai wakionyesha cheti cha ubora wa utoaji huduma kimataifa kwa wananchi (ISO) wakati wa mkutano na waandishi wa habari makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Mei 29,2015.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...