Na Dotto Mwaibale
WAPENZI wa soka
nchini sasa watafaidi kwa kutazama michuano ya kombe la dunia chini ya miaka 20
mwaka 2015 moja wa moja kwenye luninga zao kupitia ving’amuzi vya StarTimes
pekee.
Michuano hiyo
ambayo itaanza kutimua vumbi tarehe 30 mwezi Mei na kumalizika tarehe
20 mwezi Juni mwaka huu moja kwa moja kutoka nchini New
Zealand ambapo timu 24 za vijana kutoka mataifa mbalimbali duniani
yatachuana kuwania ubingwa.
Akizungumza baada
ya kupata haki miliki kutoka kwa FIFA za kutangaza michuano hiyo maarufu
duniani ambayo hubeba mastaa wa baadae kwa timu zao za taifa, Makamu wa Rais wa
StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif amesema kuwa wanafuraha kubwa kuonyesha
michuano hiyo kwani soka ni mchezo unaopendwa zaidi duniani.
“Tunayofuraha
kubwa kuwatangazia wateja wetu kuwa tumepata haki miliki kutoka FIFA za
kuonyesha michuano ya kombe la dunia kwa vijana wa umri chini ya miaka 20 mwaka
2015 itakayofanyika nchini New Zealand. Soka ni mchezo unaopendwa zaidi nchini
Tanzania na barani Afrika kwa ujumla na tunaamini tutawapatia wateja wetu
burudani ya matangazo yenye ubora wa hali ya juu kupitia ving’amuzi vya
StarTimes.” Alisema Bi. Hanif
SOMA ZAIDI HAPA
SOMA ZAIDI HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...