Mwenyekiti wa Madereva Tanzania Clement Masanja (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo katika picha) leo jijini Dar es salaam ili kuwajulisha madereva wote nchini kuwa mwaka huu wamekubaliana na Mamlaka husika kuwa hakutakuwa na mafunzo kama ilivyoelezwa hapo awali. Kulia ni Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga. Picha na MAELEZO_DAR ESALAAM

Na Pius Yalula-MAELEZO-Dar es salaam

Serikali imesema hakutakuwa na mafunzo kwa madereva wa malori na mabasi na wala hawatakiwi kwenda kusoma kozi fupi ili kuhuisha leseni zao kama ilivyokuwa imetangazwa hapo  awali na kusababisha mgomo.
Kauli hiyo imetolewa  na  Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mohamed Mpinga wakati akitoa tamko hilo kwa waandishi wa habari leo mjini Dar es salaam.

Alisema kuwa madereva wenye daraja E, C, C1, C2 na C3 walitakiwa kupata mafunzo ya muda mfupi kila baada ya miaka 3 kulingana na kanuni ziliandaliwa mwaka 2014 kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra),Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA),Chuo cha Taifa ya Usafishaji(NIT), Vyama vya Madereva , Ofisi ya Mwanasheri Mkuu wa Serikali na Chama cha Wamiliki wa Magari ya Mizigo Tanzania (TATOA) , lakini kwa mwaka huu hawatatekeleza kanuni hiyo.

Kamanda Mpinga alisisitiza kuwa kanuni hiyo hatatumika mwaka huu badala yake madereva wataendelea na utaratibu wao wa zamani wa kubadilisha na kuhuisha leseni zao kwa zile ambazo zitakuwa zimekwisha bila kuulizwa vyeti.

Aliongeza kuwa hadi hivi sasa mitala ya mafunzo hayo ya muda mfupi bado haijakamilika na wala Serikali haijawahi kupanga ada za mafunzo hayo , kwa hiyo utaratibu wa zamani utaendelea kutumika kama ulivyokuwa hapo awali.

Kamanda Mpinga alitoa wito kwa madereva wote kuwa wavumilivu kwa matatizo yao wakati Kamati ya kudumu ya kutatua matatizo ya sekta ya usafishaji ikendelea kuyatafutia ufumbuzi.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo ametoa wito kwa wananchi na wasafiri kutoa taarifa kwa viongozi wa Jeshi hilo endapo wanaona Askari wao  au dereva anatenda vitendo visivyo vya kimaadili ili aweze kuchukuliwa hatua.


Alisema kuwa jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani kipo wakati tayari kupokea malalamiko ya kuyachukulia hatua ili kulinda maisha ya wasafiri na mali zao , hivyo ni vizuri wakaripoti wale wote wanaohatarisha maisha ya wenzao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 14, 2015

    Ukweli unabaki kuwa madereva wengi nchini sio competent, wengi wao wameweza kupata leseni za kuendesha magari through corrupt ways.My take - kukubaliana na madai ya madereva ni sawa na kuweka maisha ya watanzania wasiokuwa na hatia rehani.Let's our Government rule by the law and not politics.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...