Waziri wa Utalii na Mali Asili, Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb.) akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Afisa Uhamiaji, Rosemarry Mkandala wakati alipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji mara baada ya kufungua rasmi Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” mnamo tarehe 29.05.2015 yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Waziri wa Utalii na Mali Asili, Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb.) akipokea machapisho mbali mbali yanayolenga kuelimisha jamii taratibu za Utoaji wa Huduma za Uhamiaji nchini, mapambano dhidi ya Uhamiaji Haramu na makosa mengineyo ya Kiuhamiaji, wakati alipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Maafisa wa Uhamiaji wakitoa Elimu juu ya masuala mbali mbali ya Kiuhamiaji nchini kwa wananchi na wadau mbali mbali walipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji wakati wa Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...