Kampuni ya Simu Tanzania(TTCL) kuwapatia wananchi waishio vijijini zaidi ya Laki Moja mawasiliano ya Simu ifikapo mwaka 2016. Jumla USD 3.3 (sawa na Bilioni 6.8 Tsh) zitatumika kwa ajili ya kupeleka mawasiliano kwenye kata 41 zenye vijiji 41 kupitia ruzuku kutoka kwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote(UCSAF) ikiwa ni awamu ya 2B.

Kata hizo ni pamoja; Oljoro –Arusha, Olmotonyi- Arusha, Olorieni – Arusha, Chikola- Dodoma, Mpalanga- Dodoma, Farkwa-Dodoma, Iduo-Dodoma, Masagalu-Tanga, Mazinde- Tanga , Mpale-Tanga, Misalai-Tanga, Ivaeny- Tanga, Kashisha-Tanga, Kashisha-Tanga, Arri-Manyara, Ayasanda-Manyara, Sigino-Manyara, Lengatei-Manyara, Bashay- Manyara, Buhendangabo- Kagera, Nyakato-Kagera, Ihembe- Kagera, Mwandu- Mwanza, Kiloleli- Simiyu, Itinje-Simiyu, Isanzu-Tabora, Neruma- Mara, Rigicha- Mara, Bwanga-Geita, Kasenga-Geita, Lumuli-Iringa, Kihesa-Iringa, Namichiga- Lindi, Galula-Mbeya, Luwalaje- Mbeya, Mbangala-Mbeya,Namkukwe- Mbeya, Kajunjumele- Mbeya, Kapele- Mbeya Mdandu-Njombe, Liparamba-Ruvuma.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa akizungumza na wadau wa makampuni ya simu pamoja na wananchi waliohudhuria uwekaji wa saini wa kupeleka mawasiliano vijijini.
Katibu Mkuu wa Wizara wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Patrick Makungu akitoa hotuba katika hafla ya uwekaji wa mikataba ya kupeleka mawasiliano ya simu vijijini.
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dr. Kamugisha Kazaura akitoa neno la shukhurani kwa niaba ya Makampuni ya Simu, baada ya makampuni hayo kushinda zabuni ya kupeleka mawasiliano kwenye jumla ya kata 117.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...