Baadhi ya wanawake wa kituo cha “Mabinti” kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, chini ya Hospitali ya CCBRT wakiwa darasani kujifunza elimu ya ushanoaji wa aina mbalimbali za vitu baada ya kutibiwa na kupona Fistula kupitia mradi wa matibabu unaofadhiliwa na Vodacom Foundation. Kituo hicho kinawawezesha mabinti hao kupata elimu ya kazi za mikono ili waweze kujikimu kimaisha pindi wanaporudi makwao.
Mmoja wasichana wa kituo cha “Mabinti” aliyepata kutibiwa Fistula na kupona katika Hospitali ya CCBRT Cherry David ( kulia) akiwaonesha maofisa wa Vodacom Foundation moja ya mkoba alioushana wakati walipotembelea katika kituo hicho kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam kuangalia maendeleo ya wanawake hao baada ya matibabu. Kituo hicho kinawawezesha mabinti hao kupata elimu ya kazi za mikono ili waweze kujikimu kimaisha pindi wanaporudi makwao.
Mratibu wa Kituo cha Mabinti Center kilichopo chini ya Hospitali ya CCBRT Bi. Katia Geurts akiwaelezea maafisa wa Vodacom Foundation shughuli zinazofanywa na kituo hicho wakati walipotembelea kituo hicho kuangalia maendeleo ya wanawake hao baada ya matibabu. Mabinti hao wanapata elimu ya kazi za mikono mara baada ya kupona Fistula baada ya matibabu katika Hospitali ya CCBRT ili waweze kujikimu kimaisha wakati wanaporudi makwao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...