Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais , Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani ( kati kati) akisisitiza jambo.

 Katibu Mkuu wa TSSA, Meshack Bandawe ( kushoto ) akiwa na mwezeshaji wa mafunzi, Patrick Ngwila.

Na John Nditi, Morogoro

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani, ameitaka Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kuelekeza nguvu zao vijijini kwenye idadi kubwa ya  wananchi na wazalishaji wa mali wanaohitaji huduma zao badala ya kung’ang’ania mijini pekee.

Kombani alitoa changamoto hiyo wakati akifungua mafunzo ya siku nne yaliyoanza Mei 25 hadi kufikia 28, 2015 mjini Morogoro ya  kuwajengea uwezo na ufahamu wafanyakazi wanaunda Jumuiya ya Hifadhi ya Jamii Tanzania (TSSA) kutoka katika mifuko ya Hifadhi ya jamii ya PPF,NSSF,LAPF,GEPF,NHIF na ZSSF.

Hata hivyo alisema,  mifuko hiyo imekuwa ikikimbilia kutafuta wanachama katika maeneo ya mijini na kushindwa kubuni mbinu mbadala za kuwafikia wananchi wengi wanaoishi vijijini.

Kwa mujibu wa Waziri huyo kuwa, dhana iliyojengeka kutoka kwa Mifuko hiyo kuwa vijijini hakuna watu wenye vipato sasa imepitwa na wakati kwa kuwa wananchi wanaishi vijijini  ni wakulima, wafugaji na  wafanyabiashara ndogo ndogo ambao  wanaouwezo mkubwa wa kuchangia mifuko hiyo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...