Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernald Membe akizungumza wakati akifungua Barazala Wafanyakazi la Wizara ya Mambo ya Nje katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernald  akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi lililofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi wakiwa katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Picha na Avila Kakingo,Globu Ya Jamii.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

WIZARA ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ndio inapika viongozi bora hivyo watumishi wa wizara hiyo wametakiwa kufanya kazi kwa weledi  katika kupata mafanikio ya nafasi mbalilmbali.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernald Membe wakati wa akifungua Baraza la Wafanyakazi la Wizara hiyo,amesema wafanyakazi wafanye kazi kwa weledi kutokana na wizara hiyo inavyopika watu kuwa viongozi.

Membe amesema sehemu kubwa ya wafanyakazi Ikulu wanatoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, hiyo ndio inaonekana ni jinsi gani viongozi wanapikwa katika wizara hiyo.

Amesema ikitokea anapata ajira baada ya hapo atatafuta wafanyakazi wa wizara ya mambo ya nje kutokana na upukwaji wa bora wa uongozi katika wizara hiyo.

Membe ametumia baraza hilo kwa kuaga na kuwataka wafanyakazi kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura  ili waweze kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...