Akiwa njiani kwenda Hanoi, Vietnam, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais ( Kazi Maalum),Profesa Mark Mwandosya, amekutana na  Edson Arantes do Nascimento (Pelé) mwanamichezo maarufu sana duniani. Pelé atatimiza umri wa miaka 75 ifikapo tarahe 23 Oktoba,2015. Katika uhai wake, Pelé aliweza kuingiza magoli 1283 katika michezo ya ushindani wa mpira wa miguu. 

Pelé aliichezea timu yake klabu ya Santos, Brazil kuanzia mwaka 1956 mpaka mwaka 1974.Baada ya kustaafu alijiunga na klabu ya New York Cosmos kwa muda mfupi kuanzia mwaka 1974 mpaka 1977. Pelé ametajwa kuwa mmoja wa watu maarufu zaidi duniani na hakika mwanasoka maarufu kuliko wote karne ya 20. 

Waziri Mwandosya alimshukuru Pelé kwa kuwa mfano bora katika mwenendo, maisha, ubunifu,na uongozi katika tasnia ya michezo na alimtakia afya njema na maisha marefu. Amewahi kuwa Waziri wa Michezo,Brazil. Katika picha ni Waziri Mwandosya, kulia;Pelé,katikati;na Mama Lucy Mwandosya, kushoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...