Mkutano wa 39 wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) uliofanyika katika Makao Makuu ya Shirikia hilo jijini Roma hapo tarehe 6 -13 Juni, 2015 umemchagua tena Balozi Wilfred Joseph Ngirwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la FAO (Independent Chairperson of the FAO Council - ICC) kwa kipindi cha miaka miwili (2015-2017). 

Katika Mkutano huo ambapo ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Naibu Waziri (NW) wa Kilimo Chakula na Ushirika, Mhe. Godfrey Weston Zambi (Mb), Balozi Ngirwa alikuwa mgombea pekee kama ilivyokuwa Juni, 2013 aliposhinda kwa kishindo pia na kushika nafasi hiyo kwa mara ya kwanza kwa kipindi cha miaka miwili (2013 - 2015).
Kuchaguliwa kwa balozi Ngirwa ni mwendelezo wa mafanikio ya diplomasia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na umakini wa Serikali katika kuteua wagombea wa nafasi kama hizo za kimataifa wenye sifa, uzoefu na umahiri usiomashaka katika nyanja husika. Hakika hayo ni miongoni mwa mambo yaliyo mpamba siku zote Balozi Ngirwa pamoja na sifa na uzalendo wake kama Mtanzania. Aidha, kwa ufahamu wake wa kina wa maboresho yanayoendelea kutekelezwa katika FAO, umahiri na uwezo wake mkubwa wa kuongoza vikao na kupata mwafaka (consensus), ukiwemo mwafaka kwa mara ya kwanza wa viwango vya Bajeti, vimewezesha Baraza la FAO kufikia mafanikio mengi na mkubwa chini ya uenyekiti wake katika awamu yake ya kwanza ya miaka miwili (2013 – 2015). Tunamtakia Balozi Ngirwa, na Baraza la FAO, mafanikio makubwa zaidi katika kipindi cha mwaka 2015 – 2017.
Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 39 wa FAO uliofanyika Roma 6 – 13 Juni 2015, Mhe. Godfrey Weston Zambi (Mb), NW Kilimo Chakula na Ushirika, akitoa hotuba ya Tanzania kushukuru nchi wanachama wa FAO kwa kumchagua Balozi Wilfred Joseph Ngirwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la FAO (ICC) kwa kipindi cha pili mfululizo (2015 – 2017) cha miaka miwili. Walioketi nyuma ya NW, kuanzia kushoto ni Dkt. James Alex Msekela, Balozi wa Tanzania nchini Italia na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya Chakula (FAO, WFP na IFAD), akifuatiwa na Dkt. Budeba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Kushoto mwa NW ni Balozi Neil Briscoe wa UK.
 Mkutano wa 39 wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) uliofanyika katika Makao Makuu ya Shirikia hilo jijini Roma hapo tarehe 6 -13 Juni, 2015 umemchagua tena Balozi Wilfred Joseph Ngirwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la FAO (Independent Chairperson of the FAO Council - ICC) kwa kipindi cha miaka miwili (2015-2017). Katika Mkutano huo ambapo ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Naibu Waziri (NW) wa Kilimo Chakula na Ushirika, Mhe. Godfrey Weston Zambi (Mb), Balozi Ngirwa alikuwa mgombea pekee kama ilivyokuwa Juni, 2013 aliposhinda kwa kishindo pia na kushika nafasi hiyo kwa mara ya kwanza kwa kipindi cha miaka miwili (2013 - 2015).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...