Kwa mara ya kwanza Facebook imefungua ofisi yake barani Afrika, Johannesburg nchini Afrika kusini ikiwa ndio makao makuu.


Mwanadada Nunu Ntshingila ndiye atakae ongoza ofisi hiyo itakayo jikita katika kutafuta njia mbali mbali za kuongeza ushirikiano na wafanya biashara wa barani humo.

Tayari watumiaji wa facebook barani Afrika ni milioni 120, ofisi hiyo mpya inalenga kuongeza idadi ya watumiaji wake nchini Kenya, Nigeria na Afrika Kusini.

Nunu Ntshingila ndiye mkurugenzi mkuu wa ofisi hiyo ambae amesema kuwa mkakati wa kupanua uwekezaji wao hasa katika matangazo ni mipango mikubwa ya kutanua biashara pamoja na bara la Ulaya na maeneo ya Mashariki ya Kati.

Barani Afrika kuna mtumiaji mmoja kati ya watano wa intanenti na inatarajiwa idadi hiyo kukua mara mbili zaidi kwa watumiaji wa simu za mkononi ifikapo mwaka 2020.

Asilimia 80% ya wanao tumia facebook ni wale wenye kupata huduma hiyo kupitia simu zao za mikoni.

Facebook anasema pia ina mipango madhubuti ya kuongeza wateja kutoka nchi za Senegal, Ivory Coast, Ghana, Tanzania, Rwanda, Uganda, Zambia, Msumbiji na Ethiopia ili kufikia malengo yake.
Kwa msaada wa mtandao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...