Na  Bashir  Yakub.
Wakati  mwingine  waliokopa  kwa  kutumia  viwanja /nyumba   huwa  na  mahitaji ya  kuviuza.  Wasiwasi  wao mkubwa  huwa  ni kwa  mtoa  mkopo  iwapo akijua  eneo  lililowekwa  dhamana  limeuzwa  . Pia  wanunuzi  wa  maeneo  ambayo  yamewekwa  dhamana  nao  wakati  mwingine  huwa  na wasiwasi  juu kununua  maeneo  kama   hayo.  

Nilwahi  kueleza  namna  ya  kununua  ardhi  iliyowekwa  mkopo japo  sicho  ninachozungumza  leo. Leo naeleza  hadhi  ya  kisheria ( legal  status)   kwa watu  wa  aina  tatu. Kwanza sheria  inasemaje   kwa  aliyechukua  mkopo  na kuweka  dhamana  nyumba/kiwanja  na  sasa  anataka  kuuza  eneo  hilo  japo hajamaliza  mkopo. Pili  sheria  inasemaje  kwa  mtoa mkopo  ambaye  anagundua  kuwa  eneo  alilopewa  kama  dhamana  na  akatoa  hela  limeuzwa  bila  kupewa  taarifa. Tatu  Sheria  inasemaje  kwa  huyu  aliyeuziwa  eneo  lenye  mkopo. 

1.KUUZA  NYUMBA/KIWANJA  CHA  DHAMANA.
Kwanza  ieleweke  vyema  kuwa  si  dhambi  hata  kidogo  kuuza   eneo  uliloweka  dhamana   ikiwa  hilo  litafanyika kwa  kuzingatia  misingi  maalum  ya  kisheria.  Kifungu  cha 68  cha  Sheria ya  Ardhi  kimezungumzia  habari  hii  kwa  namna   fulani.  Kubwa  zaidi  unapokuwa unaamua kuuza  eneo uliloweka  dhamana  wakati  ukijua  hujamaliza  deni    ni  kuhakikisha   haufanyi  hivyo  kwa  hila.  Uza   lakini  isiwe  kwa  hila. 

Kuuza  kwa  hila  kwa  maana  hii  hapa  ni  kuuza  ambako  kunalenga   kukwepa  kutolipa deni.Haya  yanatokea   sana,  mtu  anajua  ana  deni  na   eneo  lake  litauzwa  muda wowote  basi  anaamua  kuuza    akiamini  kuwa  yule  anayenunua  atajuana  na  watu  wa  mkopo  kwakuwa  yeye atakuwa  amekimbia  au  vinginevyo. Huku  ndiko  kuuza  kwa  hila.  Aidha  sheria   imeeleza  kuuza kutokuwa  kwa  hila  ambako ni kuuza  kwa kumshirikisha   mtoa  mkopo. Inatakiwa mtoa  mkopo  awe  amearifiwa  na  akijua  kila  hatua ya kinachoendelea.   Hii  ni kwasababu  pia  mwisho  wa  siku  mtoa  mkopo  atatakiwa  kukabidhi  kwa  mnunuzi  nyaraka  ya kununulia ardhi  kwakuwa  anakuwa  nayo  yeye  ikilinda  deni. 

2.  JINAI  KWA  KUUZA  ENEO  LA  DHAMANA.
Wengi  wanaouza  maeneo  waliyoyaweka  dhamana  bila  kutoa  taarifa  kwa  watoa  mikopo   huwa  wanatenda  jinai  ya  kughushi.  Hii  ni  kwasababu   unapomuuzia  mtu  ardhi  ni  lazima  umpatie  nyaraka iwe  hati, leseni  ya  makazi, ofa  au  hata  mkataba  wa  kununulia ( sale  agreement).  

Na  ikiwa  mtu  amechukua  mkopo  na  hajamaliza  kulipa  basi  nyaraka  hii  huendelea  kuwa  mikononi  mwa  mtoa  mkopo. Kutokana  na  hilo  ina  maana  mtu  huyu akiuza  atakuwa  hana  nyaraka  yoyote  na  akiwa  nayo  basi  ni  ya  kughushi . Mara  nyingi  haya  hujitokeza  maeneo  ambayo  hayana  hati  wala  leseni  za  makazi  ambapo   huwa  rahisi  kwa  mtu  kuandaa  mkataba  wa  kununulia  na  kumkabidhi  mnunuzi  kwa hadaa  kuwa  ndio  alionunulia.  Hii  ni  jinai  kubwa  sana  ambayo  huadhibiwa  vikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...