Dkt. Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (akiwakilisha Tanzania) katika picha ya pamoja na washiriki wa kikosi kazi cha “African Ministerial Conference on Meteorology (AMCOMET) Technical Task Force on African Regional Space Programme on Meteorology” Geneva, Uswisi tarehe 10 juni 2015.


Tanzania ambayo ni mwenyekiti wa kikosi kazi cha “African Ministerial Conference on Meteorology (AMCOMET) Technical Task Force on African Regional Space Programme on Meteorology” iliongoza kikao cha kikosi kazi hicho kilichofanyika tarehe 10 Juni 2015 sambamba na Mkutano Mkuu wa 17 wa Shrikika la Hali Duniani (WMO-CONGRESS-17)  huko Geneva nchini Uswisi. Kikao kiliendeshwa chini ya Dkt. Agnes Kijazi kwa mafanikio makubwa.
Mkutano huo wa kikosi kazi ulifanyika kwa kutumia fursa ya kuwepo washiriki katika Mkutano Mkuu wa 17 wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO Congress-17).  Lengo la mkutano lilikuwa kubadilishana uzoefu na nchi ambazo zimepiga hatua katika masuala ya hali ya hewa katika anga za juu (Space Meteorology). Aidha kikao pia kilijadili upatikanaji wa vyanzo vya mapato ambavyo vitasaidia kufanikisha programu hii na miradi itakayofanyika wakati wa utekelezaji wa program hii. 
Dkt. Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ambaye pia ni mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na mwenyekiti wa mkutano huo akiendesha Mkutano wa Kamati ya Kikosi Kazi cha Programu ya anga za juu ya AMCOMET, Geneva, Uswisi. Kulia kwake ni Dkt. Joseph Kanyanga kutoka Zambia akiwakilisha AMCOMET Bureau na Dkt. Amosi Makarau, Rais wa RA1; Kushoto kwake ni wawakilishi wawili wa Sekretarieti ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO Secretariat). 

IMETOLEWA NA: MONICA MUTONI-AFISA MAHUSIANO TMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...