Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua rasmi Chanjo ya watoto kuzuia maambukizi ya magonjwa katika kata ya Nyakisasa kijiji cha Kashinga akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Ngara mkoani Kagera,lengo la ziara hiyo likiwani ni kukagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010 na kuhimiza uhai wa chama, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na ktibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na viongozi mbalimbali wa CCM kutoka mkoa wa Kagera.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi mbalimbali za waliokuwa wanachama wa Chama cha CHADEMA mara baada ya kurejesha kwake na kujiunga na CCM katika mji wa Rulenge.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ngara Mama Constansia Buhie wakizikusanya kadi mbalimbali za wafuasi wa upinzani na kuzikabidhi kwa viongozi hao wa CCM,ikiwa ni ishara ya kujiunga na chama hicho cha CCM
Baadhi ya kadi zilizorejeshwa kwa Kinana na wananchi hao na kujiunga na CCM.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mhandisi wa kampuni ya kichina ya TKPE Bw.Ton Minyang wakati alipokagua ujenzi wa Mtambo wa umeme vijijini REA unaojengwa katika kijiji cha Djuruligwa kata ya Kabanga wilayani Ngara.
Wananchi wa Ngara mjini wakishangilia jambo katika mkutano wa hadhara wa CCM
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Abdulrhaman Kinana akiwahutubia wananchi wa Ngara mjini,Kinana ameitaka Serikali kurahisisha utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara , madereva wa magari na bodaboda badala ya kuacha watu wanasumbuka kutafuta leseni umbali mrefu tena kwa gharama kubwa.
Kinana amesema kuwa moja ya ombi la wananchi hao ilikuwa ni kuomba kurahisishiwa kupata leseni ili kuondoa usumbufu wanaoupata sasa.Alisema Serikali lazima iweke mazingira mazuri ya kutoa leseni kwa wananchi wakiwamo wafanyabishara na madereva bodaboda huku akieleza hakuna sababu ya kutumia gharama kubwa kwa ajili ya leseni.
KATIBU
wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa mji wa
Ngara Mjini kwenye mkutano wa hadara,Nape Nnauye alisema kuwa hakuna
sababu ya Watanzania kuingia kwenye mpasuko kwa sababu ya mchakato wa
katiba mpya na kuashauri ni vema mjadala ukafungwa kwenye nyumba za
ibada. Amesema inasikitisha unapoona baadhi ya viongozi wa dini badala
ya kuhubiri neno la Mungu na kuwaunganisha Watanzania wanatumia nafasi
yao kuwagawa wananchi kwa sabababu ya Katiba mpya.
PICHA NA MICHUZI JR-NGARA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...