Na Kileo Y
Ijumaa 26 – 06 – 2015 nilishiriki katika mjadala ulio jadili uchumi wa kidigitali katika kongamano lililo andaliwa na COSTECH ambapo kwa upande wangu niliangazia uhalifu mtandao unavyoweza kuleta athari kwenye uchumi wetu ukizingatia sasa miamala mingi ya kifedha imekua ikifanywa kwa msaada wa TEHAMA ( Simu, ATM , Mitandao). 

Nilitolea ufafanuzi hali halisi kwa sasa na tuendako huku nikitolea mfano uchumi wa taifa lolote unavyoweza kuyumbishwa au kudondoshwa kabisa wa endapo wahalifu mtandao watahujumu TEHAMA zinazotumika kurahisisha shughuli za kibiashara zinazokuza uchumi wa taifa.

Aidha, Nilitolea ufafanuzi mambo muhimu yakuzingatia ili kujiweka salama kimtandao – Baada ya mjadala huo nilipokea maswali mengi yaliyolenga kutaka kufahamu zaidi kuhusiana na uhalifu mtandao pamoja na kutaka nitolee ufafanuzi zaidi angalizo muhimu zinazoweza kuboresha hali ya usalama mitandao. 
Hapa Nitaangazia mambo kadhaa walau kwa uchache ya kuzingatia utumiapo mitandao situ wakati wa kufanya miamala ya kibiashara bali nitatolea na majibu ya maswali ya msingi niliyopata kuulizwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...