DSC_0080
Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akisoma hotuba ya uzinduzi wa maabara itembeayo kwa ajili ya mafunzo ya upasuaji. Kulia ni Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews na kushoto ni Mkurugenzi wa ECSA anayeshughulikia Afya ya jamii Prof Yoswa Dambisya.

Na Mwandishi wetu
Mganga Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Magreth Mhando mwishoni mwa juma alizindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.

Alifanyakazi hivyo kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii, Dk Seif Rashid.

Maabara hiyo ambayo ni mradi wa majaribio wa chuo hicho wenye lengo la kufundisha wapasuaji pale walipo imegharimu dola za Marekani 100,000.
Kwa mujibu wa taarifa za COSECSA maabara hiyo itakuwa nchini kwa miezi kama mitatu kabla ya kwenda Kenya na baadae Malawi.

Mradi huo wenye lengo la kufundisha wapasuaji zaidi kwa kufika eneo ambalo wanafanyia kazi, ni moja ya miradi ya chuo kitembeacho ambacho toka kimeanzishwa mwaka 1990 kimeshatoa wapasuaji 200.

Hafla ya uzinduzi wa maabara hiyo yenye vifaa vya kisasa vya kufundishia na kufanyia upasuaji ikiwamo ya upasuaji kwa kutumia darubini ulifanyika katika hospitali ya kumbukumbu ya Hubert Kairuki.
DSC_0053
Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo akisoma taarifa kwa mgeni rasmi kabla ya uzinduzi.
DSC_0087
Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akikata utepe kuzindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.
DSC_0097
Mmoja wa walimu ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando aliyemwakilisha Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews.
DSC_0047
Maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...