Mganga
Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akisoma
hotuba ya uzinduzi wa maabara itembeayo kwa ajili ya mafunzo ya
upasuaji. Kulia ni Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews na
kushoto ni Mkurugenzi wa ECSA anayeshughulikia Afya ya jamii Prof Yoswa
Dambisya.
Na Mwandishi wetu
Mganga
Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Magreth Mhando mwishoni
mwa juma alizindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea
iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.
Alifanyakazi hivyo kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii, Dk Seif Rashid.
Maabara
hiyo ambayo ni mradi wa majaribio wa chuo hicho wenye lengo la
kufundisha wapasuaji pale walipo imegharimu dola za Marekani 100,000.
Kwa mujibu wa taarifa za COSECSA maabara hiyo itakuwa nchini kwa miezi kama mitatu kabla ya kwenda Kenya na baadae Malawi.
Mradi
huo wenye lengo la kufundisha wapasuaji zaidi kwa kufika eneo ambalo
wanafanyia kazi, ni moja ya miradi ya chuo kitembeacho ambacho toka
kimeanzishwa mwaka 1990 kimeshatoa wapasuaji 200.
Hafla
ya uzinduzi wa maabara hiyo yenye vifaa vya kisasa vya kufundishia na
kufanyia upasuaji ikiwamo ya upasuaji kwa kutumia darubini ulifanyika
katika hospitali ya kumbukumbu ya Hubert Kairuki.
Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo akisoma taarifa kwa mgeni rasmi kabla ya uzinduzi.
Mganga
Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akikata
utepe kuzindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa
kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.
Mmoja
wa walimu ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji akitoa maelezo kwa mgeni
rasmi Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth
Mhando aliyemwakilisha Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na Naibu Balozi
wa Ireland nchini, Maire Matthews.
Maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...