TANGAZO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS – MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
inawakaribisha wananchi na wadau wote katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Tarehe 16-23 Juni, 2015
inawakaribisha wananchi na wadau wote katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Tarehe 16-23 Juni, 2015
Mahali: Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam
Kaulimbiu: “Utumishi wa Umma katika Bara la Afrika ni Chachu ya Kuwawezesha Wanawake, Kuongeza Ubunifu na Kuboresha Utoaji Huduma kwa Umma”.
Ushauri na Huduma mbalimbali zitatolewa na wataalamu kutoka katika Taasisi za umma bila malipo.
Ufunguzi utafanywa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mh. Celina O. Kombani (Mb), na siku ya kilele Tuzo zitatolewa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mh. Ali Hassan Mwinyi.
Tarehe 17 Juni, 2015 Kongamano la Wiki ya Utumishi wa Umma litafanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) na ufunguzi utaongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue, na Msemaji Mkuu atakua Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Balozi Dkt. Matern Lumbanga.
Hakuna kiingilio katika maadhimisho haya, wananchi wote mnakaribishwa.
Limetolewa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
K.n.y; KAIMU KATIBU MKUU (UTUMISHI).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...