Mwenyekiti wa klabu ya Gymkhana Dioniz Malinzi akipiga mpira wakati wa ufunguzi wa mchezo wa gofu kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa maktaba na vifaa vya kompyuta vya Shule ya Sekondari ya Mtakuja.

Na Beatrice Lyimo- Maelezo

Bahari Rotary Klabu ikishirikiana na HANSA GROUP wamefanya harambee ya tano kwa ajili ya kuchangia Shule ya Sekondari Mtakuja iliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam.

Harambee hiyo iliyofanyika katika Viwanja vya Gymkhana kwa kuwa shindanisha washiriki kucheza mchezo wa Gofu kwa lengo la kukusanya kiasi cha Shilingi Milioni 40 za kitanzania kwa ajili ya kutatua changamoto zinazoikabili shule hiyo ikiwemo Maktaba ya shule na Maabara.

Akizungumza na waandishi wa habari Rais wa Klabu hiyo Bw. Ally Abdallah alisema kuwa Shule ya Sekondari Mtakuja ina wanafunzi 1,141 na inakabiliwa na ukosefu wa Maabara ya mafunzo kwa vitendo, vitendea kazi, viti, meza, pamoja na madawati.

“Tumeona changamoto nyingi zinazoikabili shule hiyo na jamii inayowazunguka hivyo tumejitolea kukabiliana nazo kwani dhima ya Bahari Rotary Club ni kubadilisha jamii kwa ujumla haswa kwa changamoto zinazojitokeza kwa wanafunzi,”

“Mwaka huu tumejitoa kwa ajili ya Shule ya Sekondari Mtakuja ili kuwatengenezea mazingira mazuri ya kusoma kwani watoto hawa ni Viongozi wa kesho hivyo ni wajibu wetu kuwaanda” aliongeza Bw. Abdallah.

Awali Bahari Rotary Club ilichangisha kiasi cha shilingi Milioni 20 za kitanzania kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo ikiwemo Uzio wa ukuta na Geti, kununua Matanki ya Maji na kuimarisha mfumo mzima wa usambazaji wa maji shuleni hapo aliongeza Bw. Abdallah

Kwa upande wa Meneja Masoko wa HANSA GROUP Bw. Reuben Richard alifafanua kuwa Bahari Rotary Club imefanikiwa kusambaza maji safi na salama katika shule tofauti jijini Dar es salaam na kugundua kuwa shule nyingi jijini zinauhitaji maji safi na salama.

Fuchs Oil, Eco bank, Hansa Group, Oryx Oil, Tanzania Distilleries LTD, Satuguru Travel, Car and General, R.K. Chudasama, NAS Tyres Services Ltd, Tecnowares, Scania Tanzania Limited, Spice Net, Oilcom, Minex Logistics, Bank of India and SBS (T) Ltd ni baadhi wa wadhamini waliojitokeza kudhamini mashindano hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...