Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa,Ndugu Allan Kijazi akizungumza jambo,wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Wahariri wa Habari Tanzania,mapema leo asubuhi jijini Mwanza.Ndugu Kijazi alisema kuwa Utalii ni sekta mtambuka na inachochea ukuaji wa sekta nyingine ikiwa ni pamoja na kilimo, usafirishaji wa anga na barabara, huduma za fedha, huduma za chakula na malazi kudorora kwa sekta nyinginezo.   

Katika ufunguzi wa Warsha hiyo,Ndugu Kijazi alisema kuwa, Kauli mbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni  “Wajibu wa Vyombo vya Habari katika kukuza utalii”,aliongeza kusema kuwa pamoja na kuelezea shughuli za TANAPA, mada zitakazowasilishwa zitahusu masuala ya Utalii na Uhifadhi na namna wanahabari wanavyoweza kushirikiana na TANAPA katika kuhimiza uhifadhi na kuendeleza utalii. 

"Mada kuu nne zitawasilishwa na viongozi wa TANAPA na wanazuoni maarufu akiwemo Nd. Jenerali Ulimwengu na Dkt. Alfred Kikoti. Inatarajiwa kuwa washiriki watapata fursa ya kuchangia na mwishoni watatushauri namna ya kuboresha utekelezaji wa majukumu yetu",alisema Kijazi.
 Mkurugenzi wa Utalii na Masoko TANAPA,Bwa.Ibrahim Mussa akifafanua jambo katika Warsha ya siku tatu ya Wahariri wa Habari na Wana habari kutoka vyombo mbalimbali,inayofanyika jijini Mwanza katika hotel ya Gold Crest. Kauli mbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni  “Wajibu wa Vyombo vya Habari katika kukuza utalii”. Pamoja na kuelezea shughuli za TANAPA,aidha imeelezwa katika Warsha hiyo kuwa mada zitakazowasilishwa zitahusu masuala ya Utalii na Uhifadhi na namna wanahabari wanavyoweza kushirikiana nasi katika kuhimiza uhifadhi na kuendeleza utalii.


 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA),Ndugu Allan Kijazi pichani kati na Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa nchni (TANAPA),Pascal Shelutete akizungumza jambo na  Mkurugenzi wa Utalii na Masoko TANAPA,Bwa.Ibrahim Mussa katika Warsha ya siku tatu ya Wahariri wa Habari na Wana habari kutoka vyombo  mbalimbali,inayofanyika jijini Mwanza katika hotel ya Gold Crest. Kauli mbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni  “Wajibu wa Vyombo vya Habari katika kukuza utalii”.
 Baadhi ya Wahariri wa Habari kutoka vyombo mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika Warsha ya siku tatu ya Wahariri wa Habari kutoka vyombo mbalimbali,inayofanyika jijini Mwanza katika hotel ya Gold Crest. Kauli mbiu ya Mkutano wa mwaka huu ni  “Wajibu wa Vyombo vya Habari katika kukuza utalii”. Pamoja na kuelezea shughuli za TANAPA.


Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA),Pascal Shelutete akifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa kwenye semina hiyo mapema leo asubuhi jijini Mwanza.

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...