Mkuu wa wilaya ya Mufindi Bi MBONI MHITA amewataka wakazi wa mkoa wa Iringa kuhakikisha wanakuwa walinzi namba moja dhidi ya watu wenyetabia ya kuharibu mazingira katika maeneo yao, kwani kwa kutofanya hivyo ni sawa na kujiuwa wenyewe.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya habari na mawasiliano ya Halmashauri ya wilaya ya Mufindi Imetanabasha kuwa, mkuu wa wilaya ameyasema hayo kwenye kilele cha siku ya mazingira duniani yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Vikula Wilayani Mufindi Mkoani Iringa alipomwakilisha mkuu wa Mkoa kama mgeni rasmi.

MHITA amesema endapo wananchi hawata chukua hatua dhidi ya watu wenye tabia ya za kuvuna miti kiholela, ufugaji wa mifugo usiozingatia taratibu za kitaaluma, uchomaji moto ovyo, uharibifu wa vyanzo vya maji, uwindaji haramu na ukataji mijti ovyo, kunauwezekano mkubwa wa kutoweka kwa misitu na vyanzo vya maji nchini na kuhatarisha ustawi wa mwanadamu.
Aidha, ameyataja madhara yanayotokana na uharibifu wa mazingira kuwa ni pamoja na mbadiliko ya hali ya hewa, kuongezeka kwa hewa ya ukaa, misitu kuteketea kwa moto, kupungua kwa kiasi cha mvua na majra yake kubadilika kuongezeka kwa joto sanjari na kupungua kwa mavuno mashambani.

Kaulimbiu ya siku ya mazingira mwaka huu inasema ndoto bilioni saba. Dunia moja . Tumia rasilimali kwa uangalifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...