WADAU na wanaharakati wa maendeleo ya watoto leo wanaungana na jamii ya kimataifa kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Afrika kwa kuwahimiza wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kuingiza ajenda ya mtoto katika kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa Juni 16 kila mwaka tangu mwaka 1991 kwa lengo la kuhamasisha jamii kujadili, kutathmini na kuweka mikakati ya kuboresha maisha ya mtoto wa kiafrika kama msingi wa kujenga taifa bora.

Siku ya mtoto wa Afrika ilianzishwa na Jumuiya ya Umoja wa Afrika (OAU) na kuadhimishwa kwa mara ya kwanza Juni 16, 1991 ili kuwahimiza viongozi kujenga utashi wa kisiasa wa kushughulikia matatizo yanayowakabili watoto wa Kiafrika kwa kuweka sheria za kuwalinda pamoja na kuwajengea mazingira bora ya kuishi.

Maadhimisho ya mwaka huu yanafanyika sanjari na maadhimisho ya miaka 25 ya Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto kwa kutumia kaulimbiu isemayo,” Tuunganishe juhudi zetu kutokomeza ndoa za utotoni Afrika.

Wanaharakati na wadau wa maendeleo na haki za watoto wametumia maadhimisho ya mwaka huu kujadili na kutathmini hotuba za wanasiasa waliojitokeza hivi karibuni kutangaza nia ya kugombea urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kubaini kuwa hakuna mgombea aliyeweka bayana jinsi atakavyotetea haki za watoto.
Wagombea zaidi ya 30 kutoka Chama Cha Mapinduzi ambao wamejitokeza na kuchukua fomu za kugombea nafasi kupeperusha bendera ya CCM katika kinyang’anyiro cha kugombea urais. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...