Sehemu ya kundi kubwa la familia ya simba linaloishi pamoja maarufu kama "Super Pride" likiota jua katikati ya Mbuga ya wanyama ya Serengeti mkoani Mara. Kundi hili, ambalo aghalabu huwa na wanafamilia wapatao 21, huishi pamoja na kutumia muda  mwingi kuwinda na kulinda kinda wao ambao huwa katika hatari ya kuliwa na wanyama wadokozi kama vile fisi, na wakati mwingine madume ya Simba wanaotaka kuingia kundini kwa nguvu. Mara nyingi mmoja wa wanafamilia wa kundi hili hufungwa redio shingoni na watafiti wanaofuatilia tabia na nyendo za mfalme huyu wa mwituni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 22, 2015

    Picha ya simba imependeza, tujivunie na kukuza utalli nchini, vivutio vya utalii viko vingine na katika sehemu nyingi za nchi yetu ni kujipanga to kuhakikisha vinaendelezwa ili kuongeza mapato nchini na kuwawezesha wakulima wafanyabiashara na vyombo vya usafiri kunufaika na uchumi huu utakaoongezeka. Mikoa yetu yenye mwambao wa pwani ina uwezo wa kutengeneza fursa nzuri za utallii wa nje n ndani wakiboresha maeneo yao na huduma.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...