U13 KUTIMUA VUMBI MWANZA JUNI 7.

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF, Julai 7 mwaka huu litafungua mashindano ya vijana wenye umri chini ya miaka 13 jijini Mwanza kwa mikoa yote ya Tanzania kwa lengo la kung’amua vipaji kwa ajili ya kuunda timu ya Taifa  ya vijana wenye umri huo.

Mashindano hayo yatakayofanyika kwa kipindi cha wiki moja, yatafanyika katika viwanja vya CCM Kirumba na Alliance vyote vilivyopo jijini Mwanza, na maandalizi ya michuano hiyo yamekamilika na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa mkoa Mwanza.

Jopo la makocha litakua katika viwanja hivyo kusaka vipaji kwa lengo la kuanza kuiandaa timu ya Taifa ya vijana wenye umri wa miaka 13, ili ifikapo mwaka 2019 waweze kuiwakilisha Tanzania katika fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitakazofanyika hapa nchini.

Mapema wiki iliyopita Shirikisho la Soka barani Afrika - CAF liliipa Tanzania uenyeji wa michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 zitakazofanyika mwaka 2019.

TFF katika kuhakikisha inafanya vizuri katika soka la vijana, mapema mwezi Aprili iliendesha kozi ya waamuzi vijana jijiji Dar es salaam, ambapo vijana 36 walishiriki kozi hiyo na kutunukiwa vyeti.

Aidha TFF ina programu ya vijana chini ya miaka 15 ambayo ilianza kambi mwezi Aprili mwaka huu, na inatarajiwa kucheza michezo ya kirafiki katika mikoa saba nchini kati ya mwezi Juni na Agosti, kabla ya mwezi Disemba kusafiri katika nchi Malawi, Zambia, Zimbabwe, Bostwana na Afrika Kusini.

Kikosi hicho cha umri chini ya miaka 15 kinajiandaa na kuwania kufuzu kwa fainali za Vijana Afrika mwaka 2017 ambapo katika ziara hizo za mikoani, walimu watatumia nafasi hiyo kungamua na kuongeza vijana wengine katika  kikosi.

TFF KUZINDUA JEZI MPYA ZA TIMU ZA TAIFA

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF, kesho jumatano linatarajia kuzindua jezi mpya za timu za Taifa Tanzania, zitakazokuwa zikitumika katika michuano mbalimbali, uzinduzi huo utakafanyika katika hoteli ya JB Belmonte (PSPF) iliyopo eneo la Posta jijini Dar es salaam.

Katika hafla hiyo, TFF itawatunukia vyeti viongozi mbalimbali waliotoa mchango katika mpira wa miguu, wadhamini, wahamashisashaji pamoja na wachezaji waliochezea Taifa Stars ikiwa ni maadhimisho ya miaka 50 tangu Tanzania kujiunga na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA).


WATUNUKIWA WA VYETI VYA KUMBUKUMBU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 50, TANZANIA KUJIUNGA NA FIFA.

VIONGOZI WA KITAIFA:
1. Rais Msataafu Mwl. Julius K Nyerere
2. Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi
3. Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa
4. Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete
5. Rais Mstaafu Abeid Amani Karume
6. Rais Mstaafu Amani Abeid Karume
7.Rais Mstaafu Abdul Wakili
8. Rais Mstaafu Abdu Jumbe
9. Rais Dk. Salmin Amour
10. Rais Dk. Mohamed Shein

WENYEVITI/MARAIS FAT/TFF
11.Balozi Maggid
12. Mzee Ali Chambuso
13. Said Hamad El Maamry
14. Alhaj Muhidin Ahmad Ndolanga
15. Leodgar Chilla Tenga

WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO
149. Tommy Shitole
150. Willie Chiwango
151. Steven Rweikiza
152. Muhidin Issa Michuzi
153. John Ngahyoma
154. Mwalimu Omar
155. James Nhende



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 02, 2015

    Nadhani ni Tommy Sithole na si vinginevyo

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 02, 2015

    Hongera sana ankal.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...