
Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Bi Irina Bokova.
DUNIA endelevu haiwezi kuwapo kama hakutakuwepo na bahari yenye kuendeleza uhai.
Miezi michache kabla ya kufanyika kwa kongamano la kihistoria la COP21 (21st Conference of the Parties to the United Nations Framework Convention on Climate Change) la kutengeneza ajenda mpya ya maendeleo endelevu, ujumbe huu ulikuwa hauna tija.
Lakini sasa ujumbe huu una tija sana na muhimu sana.
Iwe nchi iko mbali na bahari au karibu, kila nchi na kila aina ya uhai hutegemea zaidi namna bahari inavyokuwa salama na yenye kutekeleza wajibu wake wa kulea uhai.
Kiukweli bahari ni kitu muhimu katika mfumo wa hali ya hewa duniani, ikiratibu kwa namna ya kipekee mabadiliko ya muda mrefu ya hali ya hewa na mfupi na pia uwepo wa hewa mbalimbali katika anga ikiwemo oksijeni tunayovuta.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...