EFM katika ubora wake wa kuhakikisha inawaletea burudani na elimu watu wa rika zote, ina kipindi kiitwacho Zama Zile, kipindi hiki cha saa tatu huwa hewani kila Jumapili kuanzia saa mbili hadi saa tano usiku.

Kipindi hiki huendeshwa na mwanamuziki gwiji  Anko John Kitime, ambaye ni mtunzi, mwimbaji, mpiga gitaa na pia ni mwanalibeneke aka blogger mahiri...

JOHN KITIME……Mwanamuziki huyu ambaye alianza kupiga katika muziki katika bendi mwaka 1968, na ambae  baba yake pia alikuwa mpiga gitaa aliyerekodi mara ya kwanza TBC mwaka 1959, amesema kuwa katika kipindi chake yeye hupiga muziki ambao aliusikia na hata kuucheza katika katika kipindi cha utoto wake na ujana wake. 
Katika kipindi hiki utaweza kusikia nyimbo ambazo si rahisi kusikika katika zama hizi na pia kujua habari mbalimbali za nyimbo hizo. 
Katika kipindi hiki cha Zama Zile pamoja na kusikia nyimbo ambazo huchaguliwa na wasikilizaji, pia utasikia muziki uliokuwa ukipigwa kabla ya kuingia vyombo vya muziki vilivyotumia umeme, muziki wa zamani kutoka mabara yote duniani ambao uliweza kupenya na kupendwa katika anga za Tanzania, muziki wa aina mbalimbali  uliopigwa nchini bila kusahau muziki wa taarab. 
 Ni hapa tu utaweza kusikia sauti ya Siti Binti Sadi muimbaji wa kike wa kwanza kuwa ‘superstar’ Zanzibar, pia hapa utasikia nyimbo kutoka bendi maarufu kutoka mikoa mbalimbali nchini, Mitonga Jazz ya Lindi, Kochoko Jazz ya Masasi, Mara Jazz, Super Veya ya Mwanza, Lake Tanganyika Jazz na Kibisa za Kigoma, Mbeya Jazz, Zaire Success ya Moshi na pia  zikiwemo bendi zilizokuwa za wanafunzi, kama Kwiro Secondary na Mkwawa high School. Hakika kipindi hiki nisafari ya kihistoria kila wiki. 
Je, unajua kuwa mtindo wa Fimbo Lugoda wa bendi ya Tancut Almasi ulitokana na mwanamuziki mmoja kucharazwa mikwaju na mpenzi wake? Ulijua kuwa mtindo wa Washawasha wa Maquis ulitokana na mcheza show wa Maquis kudondokewa na washawasha? Unajua kuwa mtindo wa Bomoa Tutajenga kesho wa Orchestra Mambo Bado ulitokana na geti kutaka kubomoka?
Usikose kusikiliza ZAMA ZILE kila Jumapili saa mbili mpaka saa tano usiku EFM 93.7fm

  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...