Askari wa Jeshi la Polisi, ASP Gabriel Mwasile (kushoto), akitoa maelezo kuhusu sare iliyokuwa inavaliwa na askari wa kike, kwa mwananchi aliyetembelea banda la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa
Uhamiaji (Sheria), Said Kamugisha , akisaini kitabu alipowasili katika banda la
Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi kushiriki katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi
wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.
Kushoto ni Violet Mwangalaba na Felix Mwagara wa Kitengo cha Mawasiliano ya
Serikali.
Afisa Probeshini na
Huduma kwa Jamii, Pendo Mtama akitoa maelezo kuhusu huduma za Probesheni na Huduma
kwa Jamii kwa Kamishna wa Uhamiaji
(Sheria), Said Kamugisha aliyeshiriki katika Maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa
Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Afisa Tawala, Idara ya Wakimbizi, Jeremia Chuma akitoa maelezo kwa Kamishna wa Uhamiaji (Sheria), Said Kamugisha, kuhusu huduma zinazotolewa kwa wakimbizi nchini, wakati wa maonyesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...