Mwenyekiti wa UWT Mufindi na mjumbe wa NEC Taifa Bi Marcelina Mkini akiwapongeza  wanawake kwa kuonyesha kumkubali
Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini wa kwanza kushoto akiwa na mkuu wa wilaya ya Mufindi Mboni Mhita na mwenyekiti wa UWT mkoa wa Iringa Bi Zainabu Mwamwindi wakati wa kongamano la wanawake wilayani Mufindi.

 WAKATI joto  la uchaguzi  mkuu likiendelea  kushika kasi ndani ya chama  cha mapinduzi (CCM) kwa  wanachama  wake kujitokeza kutia nia ya kuwania urais ,ubunge na udiwani , umoja  wa wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Mufindi umemuomba mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Marcelina Mkini kugombea nafasi ya ubunge jimbo la Mufindi  kusini .





Wakizungumza mara baada ya  kumalizika kwa  kongamano la UWT wilaya ya Mufindi wajumbe wa kongamano  hilo  walisema  kuwa  toka nchi ipate  uhuru  wake  mwaka 1961  wilaya ya Mufindi mkoani Iringa haijapata  kuwa na mbunge mwanamke  hivyo kwa uchaguzi wa mwaka  huu lazima wanawake wachukue nafasi ya  kuongoza ubunge jimbo la Mufindi kusini ambalo kwa  sasa  linaongozwa na mbunge Mendrady Kigola (CCM).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 09, 2015

    Haya safari hii ni zamu ya wabunge KUOMBWA.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 09, 2015

    Kina mama mkijisikia mnaweza muhamasiki kuchukua fomu msingoje tu viti maalumu hata nyinyi mnatosha na kuweza kuongoza.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...