Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar
Waziri
wa Afya wa Zanzibar Rashid Seif ameliagiza Baraza la Wauguzi na
Wakunga Zanzibar kusimamia kwa karibu watendaji wa kada hiyo ili waweze
kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.
Akizungumza
katika uzinduzi rasmi wa Baraza Wauguzi na Wakunga katika Chuo cha
Sayanzi ya Afya Mbweni, Waziri Rashid Seif amesema wauguzi na wakunga ni
walezi wanaoshughulikia matatizo ya watu hivyo wanatakiwa kutekeleza
wajibu wao kwa uadilifu.
Amesema
wananchi wanapofika Hospitali na vituo vya Afya wanategemea hifadhi na
kinga ya wauguzi kabla ya kuonana na daktari na kumekuwa na malalamiko
mengi kutoka kwa wananchi ambayo yanahitaji kutafutiwa ufumbuzi na
Baraza hilo.
Mrajisi wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar Haji Haji
Khamis akieleza mchakato wa kulisajili Baraza la Wauguzi na Wakunga katika uzinduzi rasmi uliofanyika Chuo cha
Sayansi ya Afya Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza mgeni rasmi
katika uzinduzi wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar kwenye sherehe za uzinduzi
wa Baraza hilo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Picha ya pamoja ya mgeni rasmi Waziri wa Afya
Rashid Seif na wajumbe wa Baraza la Wauguzi na Wakunga mara baada ya uzinduzi
rasmi.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...