Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar           
Waziri wa Afya  wa Zanzibar Rashid Seif ameliagiza Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar kusimamia kwa karibu watendaji wa kada hiyo ili  waweze kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Akizungumza katika uzinduzi rasmi wa Baraza Wauguzi na Wakunga katika Chuo cha Sayanzi ya Afya Mbweni, Waziri Rashid Seif amesema wauguzi na wakunga ni walezi wanaoshughulikia matatizo ya watu  hivyo wanatakiwa  kutekeleza wajibu wao kwa uadilifu.

Amesema wananchi wanapofika Hospitali na vituo vya Afya wanategemea  hifadhi na kinga ya wauguzi kabla ya kuonana na daktari na kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi ambayo yanahitaji kutafutiwa ufumbuzi na Baraza hilo.
Mrajisi wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar Haji  Haji Khamis akieleza mchakato wa kulisajili Baraza la Wauguzi na Wakunga  katika uzinduzi rasmi uliofanyika Chuo cha Sayansi ya Afya Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar. 
 Baadhi ya washiriki wakimsikiliza mgeni rasmi katika uzinduzi wa Baraza la Wauguzi na Wakunga Zanzibar kwenye sherehe za uzinduzi wa Baraza hilo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Picha ya pamoja ya mgeni rasmi Waziri wa Afya Rashid Seif na wajumbe wa Baraza la Wauguzi na Wakunga mara baada ya uzinduzi rasmi.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...