Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu akizungumza na wananchi wa
Kata ya Buger wilaya ya Karatu mkoa wa Arusha leo katika ziara ya siku
moja kuzungumza na wananchi baada ya mwananchi mmoja kuuawa kwenye msitu
wa Marang unaohifadhiwa na Shirika la Hifadhi ya Taifa(Tanapa).Waziri
Nyalandu ameunda Tume ya kuchunguza mgogoro huo ambayo itatoa
mapendekezo serikalini kwa utekelezaji.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu akizungumza na mmoja
wa wananchi wa Kata ya Buger wilaya ya Karatu mkoa wa Arusha leo baada
ya kuhutubia wananchi hao na kuwahidi serikali kuwachukulia hatua askari
waliokiuka taratibu za maadili.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Arusha,Cesilia Paresso akihutubia wananchi
wa Kata ya Buger na kuitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuzingatia
sheria na wananchi kulinda Msitu wa Marang kwaajili vizazi vijavyo.
Mkazi wa Kata ya Buger,Rehema Tango akitoa kero zake mbele ya Waziri wa Maliasili na Utalii.
sehemu ya wananchi waliohudhuria mkutano huop ambao waliweza kutoa kero zao .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...