Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu kushoto wakionyesha magwanda yaliokabidhiwa kwao aiyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wilaya ya Magu,Bi. Juliana Kachilu ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi kutoka CHADEMA.Zaidi ya wananchama 53 kutoka vyama vya upinzani walijiunga na CCM wakiwemo Chadema 28 na ACT 12 na wengine kutoka vyama vingine.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea magwanda ya aliyekuwa  Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) Wilayani Magu  Bi. Juliana Kachilu ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi, kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi zilizokuwa  za wanachama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo na vyama vingine mara baada ya wanachama hao kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kituo cha mabasi cha Kisesa wilayani Magu mkoani Mwanza.

Katibu Mkuu huyo amempokea aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) Wilayani Magu  Bi. Juliana Kachilu ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi , Kinana yuko katika ziara ya kikazi  ya mkoa Mwanza akimalizia mkoa wa mwisho wa Tanzania baada ya kuzunguka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani akipita katika majimbo yote, wilaya zote hapa nchini  na nusu ya Kata na vijiji kwa muda wa miaka miwili akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015.

Kinana amesikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzipatia ufumbuzi huku akihimiza uhai wa CCM ambapo pia  katika ziara hiyo amekuwa akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye . 
Baadhi ya Kadi za wafuasi wa vyama mbalimbali walizoamua kuachia ngazi na kuhamia chama CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu  Kinana akiwahutubia wakazi wa mji wa Kisesa mapema jioni ya leo alipokuwa akimaliza ziara yake ndani ya jimbo la Magu.


 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo akizungumza na wananchi kuhusu kuiagiza mamlaka ya Mapato TRA na kikosi cha Usalama Barabarani kuenda katika wilaya kwa ajili ya kutoa huduma za utoaji wa leseni za uendeshaji vyombo vya moto na kukusanya kodi mbalimbali za vyombo vya moto ili kupunguza urasimu wa huduma hiyo ambazo zimekuwa zikipatikana kwenye miji mikuu ya mikoa peke yake.

PICHA NA MICHUZI JR-MAGU-MWANZA

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...