Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukivuka mto kuelekea katika kijiji cha Ilyanchele wilayani Bukombe wakati akiwa katika ziara ya kikazi katika wilaya hiyo kuelekea katika kijiji hicho hata hivyo msafara huo haukuweza kuvuka mto mkubwa wa Ilyanchele na magari  kutokana na kutokuwepo kwa daraja linalounganisha kijiji hicho ambapo leo ndiyo limewekwa  jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo  na Ndugu Abdulrahman Kinana.


Baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa daraja hilo Kinana pamoja na msafara wake walivuka mto huo kwenye daraja la miti lililotengenezwa kwa nguvu za wananchi.  kisha alipanda pikipiki na kuelekea katika mkutano mdogo na wananchi wa kijiji cha Ilyamchele ambacho kimo katika msitu wa akiba  kata ya Nyamonge wilayani Bukombe mkoani Geita.



Kinana yuko katika ziara ya kikazi katika mikoa ya Kagera, Geita na Mwanza ambapo baada ya kumaliza ziara yake mkoani Kagera sasa anaendelea na ziara hiyo katika mkoa wa Geita kabla ya kumalizia ziara yake mkoani Mwanza akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akivuka na wananchi katika daraja hilo.
Wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana alipokuwa akiwahutubia mjini Bukombe,mkoani Geita
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwahutubi Wananchi katika mkutano wa hadhara mjini, Bukombe wakati wa ziara yake mkoani Geita

PICHA NA MICHUZI JR -BUKOMBE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2015

    Hili daraja linahitaji kuboreshwa kuwa la kisasa zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...