
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Philbert Rweyemamu akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Bi Josephine Matiro jengo la maabara la shule ya Sekondari ya Mazinge ambalo limejengwa kwa ufadhili wa kampuni yaKuchimbaDhahabu ya Acacia. Anayepiga makofi ni mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Mh Steven Masele.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais na Mbunge wa Shinyanga Mjini Mh. Steven Masele akitoa maneno ya shukurani kwa kampuni ya kuchimba Dhahabu ya Acacia kwa msaada wa ujenzi wa maabara kwa baadhi ya shule za sekondari katika manispaa ya Shinyanga

Mkuu wa wilaya Shinyanga Bi Josephine Matiro akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia kukabidhiwa kwa maabara hizo ambazo zimejengwa kwa msaada wa Kampuni ya Kuchimba Dhahabu ya Acacia kupitia Mgodi wa Buzwagi.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi,Mhandisi Philbert Rweyemamu akizungumza na waandishi wahabari mara baada ya kukabidhi majengo ya Maabara hizo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...