Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akizungumza na madiwani na watendaji wa Manispaa hiyo wakati wa kikao maalum cha kuahirisha Baraza hilo kilichofanyika jana Dar es Salaam. Wengine ni Naibu Meya, Songoro Mnyonge na Mkurugenzi wa Manipss hiyo, Eng. Mussa Nati (kulia).
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akimtambulisha Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi kwa Madiwani wa Manispaa hiyo baada ya kuwasili kwenye ofisi za Manispaa hiyo kuhudhuria hafla maalum ya kuahirisha Baraza hilo Dar es Salaam jana.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akionesha cheti cha Freeman alichokabidhiwa na Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi (kushoto kwake) katika hafla hiyo. Cheti hicho kinachotolewa na Baraza la Madiwani hutolewa mara chache kwa Meya aliyefanikiwa kutekeleza miradi ya wananchi kwa kiwango kikubwa na kina maana ya ‘Raia Huru’. Kushoto ni Naibu Meya, Songoro Mnyonge na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mushi.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...