BENKI ya CRDB imewataka Watanzania kutembelea banda lao ili kupata huduma mbalimbali za Fedha.
Akizungumza katika Maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama sabasaba yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba, Ofisa wa benki hiyo, John Titus amesema kuwa banda lao linashughulika na kufungua akaunti na kumuhudumia mteja.
Aliongeza kuwa Benki ya CRDB pia imeweka Mobile Branch ambayo hufanya kazi zote zinazofanywa na benki hiyo ikiwemo huduma za kuweka fedha na kutoa.
Titus alisema pia wanahuduma ya Jumbo ambayo ni akaunti kwa ajili ya watoto.
Alisema akaunti hiyo huwapa watoto fursa ya kuwekezewa fedha zitakazowasaidia katika masomo na maisha yao ya baadae.
Wateja wa Benki ya CRDB wakipata huduma za Fedha katika Mobile Branch katika maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba Barabara ya Kilwa.
Wateja wa Benki ya CRDB wakipata huduma za Fedha katika Mobile Branch katika maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba Barabara ya Kilwa.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...